Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, October 2, 2014

IPTL YAIMWAGIA TASWA MILIONI 20 KUANDAA TUZO ZA WANAMICHEZO.



Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Sigh Seth (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 20 kwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto (wapili kulia) ikiwa ni mchango wa IPTL kusaidia maandalizi ya Tuzo za wanamichezo bora nchini. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni ni Makamu Mweyekiti wa TASWA, Egbert Mkoko, Katibu Mkuu, Amir Mhando na Mwanasheria na Mshauri Mkuu wa IPTL,Joseph Makandege na kulia ni Mjumbe wa TASWA, Rehure Richard Nyaulawa

 Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Sigh Seth akiwaeleza wanahabari furaha yake ya kuisaidia TASWA kitita hicho cha fedha kusaidia wanamichezo ambapo nae alikiri kuwa ni miongoni mwa wanamichezo na amewahi kuwa Mshindi wa tatu wa Mbio za Magari Afrika.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Sigh Seth (katikati) akiwaongoza wanahabari kuangalia mitambo ya Kampuni hiyo ambayo inazalisha umeme. Kulia ni Katibu mkuu wa TASWA, Amir Mhando na Kushoto ni Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto.
Waandishi wa habari wakiingia kuangalia uzalishaji wa umeme katika mitambo ya IPTL.
Picha na Mroki mroki

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...