Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, July 12, 2012

MATUKIO MBALIMBALI YA ZIARA YA RAIS KIKWETE NCHINI UINGEREZA


Rais Jakaya Mrisho kikwete, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda na mkewe Mama Janet Museveni, Waziri Mdogo wa Uingereza wa Maendeleo ya Kimataifa Bw. Stephen O'Brien (kulia) na Mama Melinda Gates wakibadilishana mawazo kabla ya kuhutubia katika mkutano wa kimataifa wa viongozi kujadili Uzazi wa Mpango kwa nchi masikini zaidi duniani katika ukumbi wa Queen Elizabeth II jijini London July 11, 2012. Mkutano huo ni wa kwanza wa aina yake duniani na umeanzisha Mchakato wa Dunia ambao utalenga kuwawezesha wanawake wapatao milioni 120 katika nchi masikini zaidi duniani kupata habari, huduma na mahitaji ya kupanga uzazi bora zaidi na kuokoa maisha yao ifikapo mwaka 2020.
PICHA NA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akuhutubia katika mkutano wa kimataifa wa viongozi kujadili Uzazi wa Mpango kwa nchi masikini zaidi duniani, katika ukumbi wa Queen Elizabeth II jijini London July 11, 2012. Mkutano huo ni wa kwanza wa aina yake duniani na umeanzisha Mchakato wa Dunia ambao utalenga kuwawezesha wanawake wapatao milioni 120 katika nchi masikini zaidi duniani kupata habari, huduma na mahitaji ya kupanga uzazi bora zaidi na kuokoa maisha yao ifikapo mwaka 2020.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...