Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, August 14, 2012

kampuni ya bia ya serengeti yamkabidhi Mshindi wake wa gari promosheni ya Vumbua Hazina chini ya Kizibo mjini dodoma leo


Mshindi wa gari wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro ambaye ni   mkazi wa Dodoma ambae ni mtaalamu wa mambo ya bomba,akiwasha mchuma wake tayari kuaondoka nalo huku shamra shamra za hapa na zikiwa zimetawala kutoka kwa ndugu na jamaa waliofika kwenye tukio hilo adhimu kabisa.
Mshindi wa gari wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro  akiingia ndani ya gari yake aina ya Ford Figo baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Masoko wa Serengeti Breweries Bw. Ephraim Mafuru, hafla hiyo imefanyika jioni ya leo kwenye bustani ya Nyerere Square mjini  Dodoma. Wanaoshuhudia katikati yao ni Baba yake Mzee Augustine Tengia, wengine wanaoshuhudia tukio hilo ni Allan Chonjo, meneja wa bia ya Serengeti Premium Lager sambamba na Wanahabari .
Mkurugenzi wa Masoko wa Serengeti Breweries Bw. Ephraim Mafuru  akimkabidhi kadi ya gari mshindi wa gari wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro kwenye hafla fupi iliyofanyika jioni ya leo kwenye bustani ya Nyerere Square mjini  Dodoma. Wanaoshuhudia katikati yao ni Baba yake Mzee Augustine Tengia wakiwemo Wanahabari ndugu jamaa na marafiki.
Mkurugenzi wa Masoko wa Serengeti Breweries Bw. Ephraim Mafuru  akimkabidhi funguo ya gari lake mshindi wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro kwenye hafla fupi iliyofanyika jioni ya leo kwenye bustani ya Nyerere Square mjini  Dodoma. Wanaoshuhudia katikati yao ni Baba yake Mzee Augustine Tengia wakiwemo Wanahabari ndugu jamaa na marafiki.
Meneja wa kinywaji cha Serengeti Premium Lager Bwa. Allan Chonjo akifafanua jambo mbele ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali na wadau wengine kutoka sehemu mbalimbali waliofika kulishuhudia tukio la kukabidhiwa kwa gari aina ya Ford Figo kwa mshindi wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro kwenye hafla fupi iliyofanyika jioni ya leo ndani ya bustani ya Nyerere Square mjini  Dodoma.
Mshindi wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro akifurahia zawadi hiyo na Mama yake Mzazi ambaye pia alikuwepo kulishuhudia tukio hilo lililofanyika jioni ya leo kwenye bustani ya Nyerere Square mjini  Dodoma.
Mshindi wa shindano la Vumbua Hazina chini ya Kizibo  Bw. Amin Joseph Maro akizungumza mbele ya Wanahabari waliofika kulishuhudia tukio hilo jioni ya leo kwenye bustani ya Nyerere Square mjini  Dodoma,kulia kwake ni Baba yake Mzazi Mzee Augustine Tengia.
Baba yake Mzazi Mzee Augustine Tengia akizungumzia furaha alionayo mbele ya Wanahabari mara baada ya mtoto wake kujishindia gari mpya kabisa aina ya  Ford Figo kupitia promosheni ya Vumbua Hazina chini ya Kizibo iliyokuwa ikiendeshwa na kampuni ya bia ya Serengeti.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...