Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, August 8, 2012

KCB YAMWAGA MISAADA ZANZIBAR


 Katibu Mkuu wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar,Bw.Omar Abdallah akipokea msaada wa vyandarua pamoja na mashine ya kupumlia wagonjwa(Oxygen Conamtrator)vyenye thamani ya Milioni Tano kwa niaba ya Hospitali ya Mwembeladu kutoka kwa Meneja wa  banki ya KCB Tawi la Stone Town Zanzibar Bw.Rajabu Ramia.Kulia ni Meneja wa Biashara wa Benki ya KCB Zanzibar Bw.Abdallah Mshangama.
 Katibu Mkuu wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar,Bw.Omar Abdallah kushoto akipokea Mashine ya kupumlia wagonjwa(Oxygen Conamtrator) kwa niaba ya Hospitali ya Mwembeladu kutoka kwa Afisa Uhusiano wa Benki ya KCB Tawi la Stone Town Zanzibar Bw.Said Amour,katikati Meneja wa  banki ya KCB Tawi la Stone Town Zanzibar Bw.Rajabu Ramia,Benki hiyo ilitoa msaada wa vifaa vyenye thamani ya Shilingi Milioni Tano.

 Meneja wa Benki ya KCB Tawi la Stone Town Zanzibar Bw.Rajabu Ramia,akimkabidhi Muuguzi Msaidizi wa Hospitali ya Mwembeladu Zanzibar Bi.Zawadi Suleiman Msaada wa Vyandarua pamoja na mashuka 50 na vifaa mbalimbali vyenye jumla ya thamani ya Shilingi Milioni Tano.

 Afisa Mahusiano wa Benki ya KCB Tanzania Bi. Martha Edward akimpatia zawadi ya Tende Bi.Amina Ahamed alielazwa katika Wodi ya Wazazi kwenye Hospitali ya Mwembeladu Zanzibar mara baada ya wafanyakazi wa Benki ya KCB kufika katika Hospitali hiyo kwa lengo la kutoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye jumla ya thamani ya Shilingi Milioni Tano.

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya KCB wakiwa kwenye picha ya pamoja na wauguzi wa Hospitali ya Mwembeladu Zanzibar mara baada ya wafanyakazi wa Benki  hiyo kufika katika Hospitali hiyo kwa lengo la kutoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye jumla ya thamani ya Shilingi Milioni Tano.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...