Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, August 15, 2012

MSANII MWANNE KUTOKA NA DUME MASHAUZI


MWIMBAJI  wa muziki wa Taarab Mwanne Othman Sekuru pichani juu  ambaye anatamba katika  wimbo  wa Vifuu Tundu alioshirikishwa na AT,ambao  pia ulipenya na katika  tuzo za muziki za Kilimanjaro 2012 sasa kuipua kibao kingine baada ya sikukuu ya Idd El Fitr wimbo huo unakwenda kwa jina la  ‘Midume Mashauzi.

Akizungumza leo Mwanne alisema kwamba mashabiki wake wakae mkao wa kupata raha kwani katika wimbo huo ameachia  madongo ambayo kama mtu atakuwa na tabia hizo basi dongo hilo litakuwa ni sawasawa kwa muhusika.
"Katika wimbo huo ambao tumeimba pamoja umetungwa na Mohammed Omari Mkwinda ‘Meddy’ ambaye mara baada ya kuutunga akaniletea namimi nikaweka maneno ya kutia nakshi kama, Watashindana lakini watashindwa wenyewe na mengine mengi kama ‘hunathamani kama mkia wa mbuzi hufuniki wala hufukuzi nzi’ na mengine mengi tu".
Mwanne ambaye mbali ya kuwa  muimbaji katika kundi la Jahazi Modern Taarab pia ni mtangazaji wa kipindi cha ‘Tamtam za Mwambao’ kinachorushwa katika kituo cha redio ya East Africa ‘EATV’.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...