Mkuu
wa wilaya ya Mororgoro Mh Said Ally Amanzi akisaini kitabu cha wageni
mara baada ya kuwasili kukagua maonyesho ya vijana wajasiriamali ya mkoa
wa morogoro akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni
iliyoandaa maonyeshi hayo Ndugu Jackson Audiface. Maonyesho hayo ambayo
yapo katika mpango wa kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana ujulikanao
kama Tanzania Youth Entrepreneurship Programme (TAYEP) ambao upo chini
ya kampuni ya AJ IT Development Company Ltd.
Mkuu
wa wilaya ya Mororgoro Mh Said Ally Amanzi akikagua baadhi ya bidhaa
zinazozalishwa na wajasiriamali kutoka mkoa wa morogoro. baadhi ya
vijana hao kutoka chuo kikuu cha kilimo Sokoine, Chuo kikuu Mzumbe, Chuo
kikuu cha kiislaam Morogoro. Lengo la maonyesho hayo ni kuzitangaza na
kuzitafutia masoko kazi za vijana wajasiriamali.
Mkuu wa wilaya ya Mororgoro Mh Said Ally Amanzi katika meza kuu akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni iliyoandaa maonyeshi hayo Ndugu Jackson Audiface (aliyevaa
shati jeupe) pamoja na mwenyekiti wa kikundi cha vijana wajasiriamali
wa morogoro kijulikanacho kama MOMUYO ndugu Alexander Jokonia (wa pili
kutoka kulia) pamoja na afisa tarafa wa manispaa ya morogoro Mh Pakala
Pakala (wa mwisho kulia).
Baadhi
ya washiriki mbalimbali kutoka vyuo na vikundi mbalimbali vya
wajasiriamali kutoka mkoani morogoro walioshiriki katika maonyesho hayo .
Mwakilishhi
wa serikali ya wanafunzi kutoka chuo kikuu Mzumbe Ndugu Norbert
Kabendera akitoa neno la shukrani wakati wa maonyesho hayo.
No comments:
Post a Comment