Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, August 13, 2013

CRDB YAKABIDHI WODI YA WAZAZI NA VIFAA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA META-MBEYA


 Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi wodi ya wazazi iliyofanyiwa ukarabati na benki hiyo katika Hospitali ya Rufaa Mbeya, Kitengo cha Huduma ya Akinamama na Watoto-Meta. Hafla hiyo ilifanyika mjini Mbeya, mwishoni mwa wiki. 
 Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji  wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), akipanda mti wa kumbukumbu wakati wa hafla ya kukabidhi wodi ya wazazi iliyofanyiwa ukarabati na benki hiyo katika Hospitali ya Rufaa Mbeya, Kitengo cha Huduma ya Akinamama na Watoto-Meta. Hafla hiyo ilifanyika mjini Mbeya, mwishoni mwa wiki. 
 Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe akipanda mti wa kumbukumbu katika hospitali ya Rufaa ya Meta wakati wa hafla ya kukabidhi wodi ya wazazi iliyofanyiwa ukarabati mkubwa na benki ya CRDB. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigalla na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk. Charles Kimei.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe (katikati) akimwagilia mti wa kumbukumbu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakati benki hiyo ilipokabidhi wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa Mbeya, Kitengo cha Huduma ya Akinamama na Watoto-Meta.
Zoezi la upandaji miti likiendelea. 
Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe akikata utepe wakati wa kukabidhi wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa Meta, ambayo imefanyiwa ukarabati na benki ya CRDB. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Mbeya. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk. Charles Kimei, kushoto ni Murugenzi wa tawi la Mbeya, Benson Mwakyusa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigalla.
 Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa benki ya CRDB, Tully Mwambapa akimkabidhi kasha la juisi, Salome Zakaria, ambaye ni mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya Kitengo cha Huduma ya Akinamama na Watoto-Metawakati wa hafla ya benki hiyo kukabidhi wodi ya wazazi iliyofanyika mjini Mbeya, mwishoni mwa wiki.
 Pole mama, pokea zawadi.
 Tucheze kwaito.
 Mfanyakazi wa benki ya CRDB tawi la Viwawa, Mbozi, Beatrice Kyando akimwagilia maji mti wa kumbukumbu alioupanda.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe akipaka rangi wodi ya wazazi katika hospitali ya Rufaa ya Meta, wakati wa hafla ya kukabidhi wodi hiyo kwa uongozi wa hospitali hiyo baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa na benki ya CRDB. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Mbeya.
 Mke wa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe akiwafariji wagojwa waliolazwa katika wodi ya wazazi katika hospitali ya Rufaa ya Meta.
 Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk. Charles Kimei wakati wa hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wadau na wateja wa benki hiyo iliyofanyika mjini Mbeya.
 Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza katika hafla hiyo. 
 Wafanyakazi wa benki ya CRDB pamoja na wadau wa benki hiyo wakicheza muziki.
 Tucheze mduara
 Wadau wakicheza Kwaito.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...