Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, February 1, 2014

WAZIRI MKUCHIKA AGOMA KUMUONGELEA LOWASSA NA MBIO ZA URAIS 2015


Mwenyekiti  wa  CCM Taifa Rais Dr  Jakaya  Kikwete kushoto akimnadi Lowassa jimboni kwake katika uchaguzi mkuu wa mwaka  2010
 Waziri Mkuchika (kushoto) akihojiwa na mzee  wa matukiodaima leo mjini Iringa 
..................................................................................................................................................
HUKU  baadhi  ya  makundi  yakiendelea  kuibuka na kutoa kauli mbali mbali  dhidi ya waziri mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa kuwa ameanza kampeni za Urais mapema , waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora) Ndugu George Mkuchika amesema  kuwa hajafanya  utafiti wowote juu ya Lowassa  hivyo hawezi  kuzungumzia chochote  kama ni rushwa ama lah.

Waziri mkuchika  alitoa kauli  hiyo mjini Iringa leo  wakati  akihojiwa wa wanahabari mara  baada ya  kumaliza kutoka hotuba yake ya maadili na Rushwa kwa watumishi  wa umma katika kikao cha kamati ya ushauri  (RCC) cha  mkoa wa Iringa  katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo .

Kwani  alisema Taasisi ya  kuzuiana na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) nchini  imekuwa  ikiwakamata   watu na kuwafikisha mahakakani  bila  kuogopa kiongozi ama mtu wa chini na kuwa  utendaji wa taasisi hiyo  umekuwa ukiziongatia haki kwa kila mhusika.

Mkuchika  mbali ya  kugoma  kulizungumzia suala la Lowassa bado alisema  kuwa suala la Rushwa ni suala ambalo halikubaliki na kuziagiza Halmashauri  ya   wilaya  nchini  kuchunguza mienendo  ya  watumishi ambao waongoza  kwa kumiliki  mali mara  baada ya  kuingia serikalini  ili  kujua utajiri  huo wa haraka wanaotoa  wapi.

Hata  hivyo   akihojiwa  juu ya  sakata  ya aliyekuwa mshindi wa kura  za maoni ndani ya  CCM katika mchakato wa ndani ya chama hicho mwaka 2010 Frederick Mwakalebela suala lake kuchukua muda mwingi zaidi na kurudishwa mahakamani mara kwa mara  alisema ili kuwa si kwa lengo la kumuonea ila ilikuwa ni kutafuta sheria inasemaje katika  hilo na mahakani ndicho  chombo  pekee  cha kutafsiri sheria  hivyo maamuzi ya mahakamani siku  zote ni sahihi katika kutafuta  haki.


Awali Waziri Mkuchika  akihutubia katika ufunguzi wa kikao  hicho cha RCC alisema  kuwa  mikakati ya  ofisi yake  katika  kupambana na  watumishi  wasio na maadili ambao  wanashindwa  kufanya kazi  ya umma na  kutumia ofisi  za umma kujinufaisha  wenyewe.

Alisema kuwa  iwapo  watumkishi  wa umma hawatakuwa na maadili katika  uwajibikaji  wao  wa kila  siku ni  wazi suala la rushwa katika idara  wanazoongoza  zitaendelea   kuongezeka  hivyo  kuifanya  jamii  kuendelea  kuchukia serikali  yao.

Hata  hivyo  alisema ni  vema Halmashauri  kuhakikia  kamati za maadili ya  watumishi  zinafanya kazi vema  ili  kuwabaini  watumishi  wasio na maadili  katika Halmashauri  zao.

Pia  alisema serikali  kila mwaka  imekuwa ikipelekea fedha  zaidi ya asilimia 70 kwa Halmashauri kwa ajili ya manunuzi  ila matokeo  yake  badala ya  fedha  hizo  kutumika katika manunuzi wajanja  wamekuwa  wakizitumia kujinunulia mali  zao jambo ambalo alidai  halitavumilika katika wataki  huu.

" Haiingii akilini  kuna  mtumishi ameingia katika ajira  akiwa hana hata  gari  wala nyumba ila baada ya miezi  miwili ya  utumishi  wa umma unakuta  ana nyumba za kisasa, magari  na mali  nyingi ambazo mazingira ya upatikanaji  wake yanatia  shaka .....lazima  kuwa makini  sana na maofisa ardhi na  wakuu wengine  wa  idara "

Aidha  alisema katika  kukomesha  vitendo vya  rushwa katika Halmashauri ya idara  mbali  mbali za serikali  amewaagiza makamanda wa taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU ) kuhakikisha  wanatoa  elimu kwa  mabaraza ya madiwani wa Halmashauri  zote nchini  ili  kuhakikisha vitendo vya rushwa  katika Halmashauri  vinakomeshwa.

Waziri Mkuchika  alisema  kuwa   hadi sasa kwa nchi zinazoongoza  kwa utawala bora katika  jumuiya ya  Afrika Mashariki   takwimu  zinaonyesha kuwa  kati ya nchi  tano  Tanzania ni nchi ya pili  kwa utawala  bora   .

Pia  alisema  chanzo  cha  mmomonyoko  wa maadili kwa mtumishi  wa umma  ni pamoja na tamaa ya mali  kwa  watumishi hao hali  inayosababishwa na kutoridhika na  kipato  halisi  wanachokipata pamoja na ubinafsi  wa kujitazama  wao badala ya  Taifa .

"Takwimu  kuhusiana na vita  dhidi ya  Rushwa  na  uwajibikaji kwa viongozi  unakabiliwa na changamoto  nyingi..... takwimu kuhusiana na vitendo  vya Rushwa  katika kipindi  cha kuanzia mwezi Julai 2012 hadi  Juni 2013 zinaonyesha  kuwa na jumla ya taarifa 81 zilipokelewa kati  ya hizo  65 zilifanyiwa kazi  uchunguzi  na kufunguliwa majalada .....aidha katika kipindi  hicho jumla ya kesi mpya 12 zilifunguliwa katika mahakama mbali mbali za mkoa wa Iringa na kesi 5 kati ya  hizo zilitolewa  hukumu na  wahusika kupewa adhabu mbali mbali" alisema waziri Mkuchika

Kuwa Halmashauri  ya  wilaya  pamoja na idara ya afya ndizo zinaongoza kwa kuwa na taarifa nyingi kwa upande wa idara za serikali  ambapo  kila moja ilipatikana na taarifa  16 huku idara ya mahakama  inafuatia kwa taarifa  6 wakati  polisi na idara ya  elimu zikiwa na taarifa 5 kila moja  idara ya maliasili taarifa  tatu  na idara ya mwisho kwa kuwa na taarifa  ndogo za rushwa ni idara ya ardhi  na  TANROADS ambayo ilikuwa na taarifa  moja ,Tanesco taarifa  moja,SIDO mbili,ofisi   ya mkuu wa wilaya  tatu ,na sekta  binafsi taarifa  tatu.

Mkuchika alisema kuanzia  sasa  maofisa wa Takukuru wilaya ya mkoa hakuna kushinda  ofisini na badala yake kwenda kwa  wananchi  kutoa elimu  ya Rushwa na  kuzitaka  taasisi mbali mbali zikiwemo za dini kutosita  kutoa taarifa kwa Takukuru  kuomba  maofisa  wake kufika na kutoa elimu katika mikusanyiko.

Mwenyekiti  wa Halmashauri ya  wilaya ya  Iringa Stephano Mhapa  mbali ya  kumpongeza  waziri Mkuchika kwa utaratibu  wake wa kuzunguka katika mikoa na kuzungumza katika vikao  vya RCC bado alimshauri  kufanya mikutano ya hadhara  kwa wananchi  zaidi ambao  ndio  wanaathiriwa  zaidi na rushwa ndogo  zinazoendelea  kutolewa na kuvuruga ubora wa  miradi.

Huku  mkuu  wa wilaya ya  Mufindi  Evarista  Kalalu  alisema  kuwa  mbali ya wilaya  yake ya Mufindi  kuongozana na maofisa wa TAKUKURU katika mikutano  yake wilayani ila bado  inapaswa TAKUKURU  kujipanga kwa  kutenga bajeti  ya  kufikisha  elimu zaidi kwa wananchi.

Kwani  alisema  iwapo  TAKUKURU haitakuwana nguvu zaidi  ya  kuwafikia  wananchi  wa pembezoni  zaidi  bado vita  dhidi ya  Rushwa  itaendelea  kuzungumzwa  pasipo  kueleweka  vema.

Mkuu  huyo wa wilaya  alisema Rushwa inayotesa wananchi ni ile inayotokana na uwajibikaji mbaya  wa  viongozi wa serikali  za vijiji na kata  ambao  ndio  wamekuwa  wakiongoza kwa  rushwa ndogo ndogo ambazo  zinaendelea  kutesa  wananchi .

Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dr Christine  Ishengoma  aliwataka  watumishi  wote wa umma na  wananchi wa mkoa  wa Iringa  kushirikiana katika mapambano  dhidi ya  Rushwa kama  njia ya kuongeza kasi  ya maendeleo katika mkoa.

Dr Ishengoma alisema  kuwa iwapo  kila mmoja atajikita katika vita  dhidi ya  Rushwa mkoa  wa Iringa  unaweza kuwa mkoa wa mfano kwa maendeleo makubwa bila  Rushwa

Katika hatua  nyingine  mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dr Ishengoma  aliagiza Halmashauri zote za mkoa  wa Iringa ndani ya miezi mitatu  kuitisha  semina ya utawala  bora  katika  suala la Rushwa na maadili  kwa madiwani  wake.

"Mheshimiwa  waziri napenda kukuhakikishia  kuwa tunaye  kamanda wa TAKUKURU Mzuri  katika mkoa  wa Iringa japo kamanda nakuomba usije kutia  kiburi kwa waziri  wako  kutokana na sifa  hizi  ambazo  nimepata  kukupa hapa  leo"

Kamanda  wa Takukuru  mkoa  wa Iringa Bi Emma Kuhanga  alisema kuwa  mkoa  wa Iringa  umeendelea  kupambana na vitendo  vya  Rushwa na kuwa suala la  watumishi  wanaofika na kumiliki mali nyingi  habari zao wa kwanza  kuzibaini ni wakurugenzi na maofisa  utumishi ambao ndio  wamekuwa  wakijua mienendo  yao japo alisema bado  wataendelea  kufuatilia watumishi  wanaofanya vitendo  vya ufisadi kwa ajili ya kujilimbikizia mali katika mkoa

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...