Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, March 24, 2014

SIMBA PWAAA, YAPIGWA 1-0 NA COASTAL UNION, AZAM YAZIDI KUPAA






TIMU kongwe ya soka nchini, Simba jana ilipigwa mweleka wa bao 1-0 na Coastal Union katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kipigo hicho kimepoteza matumaini ya Simba kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo baada ya kutokuwa na uwezo wa kushika nafasi mbili za kwanza.

Bao pekee na la ushindi la Coastal Union lilifungwa na mshambuliaji Hamad Juma dakika ya 44, kufuatia shambulizi kali lililofanywa kwenye lango la Simba.

Simba ilizinduka katika kipindi cha pili na kufanya mashambulizi kadhaa kwenye lango la Coastal Union, lakini juhudi za washambuliaji wake kusaka bao la kusawazisha hazikufanikiwa.

Kiungo Jonas Mkude ndiye aliyefanya majaribio mengi kwenye lango la Coastal Union kwa kupiga mashuti makali matano, lakini moja liligonga mwamba wa pembeni wa goli na mengine yalitoka nje.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa juzi, Azam iliichapa JKT Oljoro bao 1-0 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Ashanti ilipigwa mweleka wa mabao 2-0 na JKT Ruvu mkoani Pwani.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...