Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, April 13, 2014

Azam kuweka historia kwa kutangazwa mabingwa wapya?


Azam Fc
KLABU ya soka ya Azam leo kuwa Bingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014? Hilo ndilo swali linalotawala vichwa vya mashabiki wa soka nchini wakati kitimtim cha ligi hiyo kitakapoendelea tena leo kwenye viwanja vinne tofauti.
Azam ambayo haijapoteza mechi yoyote mpaka sasa katika ligi hiyo, itakuwa ugenini kwenye uwanja wa Sokoine kuvaana na wenyeji wao Mbeya City, huku mabingwa watetezi Yanga pia watakuwa kwenye uwanja wa ugenini dhidi ya Oljoro JKT jijini Arusha.
Hata kama Yanga itashinda pambano lake la Sheikh Amri Abeid kwa idadi kubwa ya mabao haitawasaidia kama Azam itashinda jijini Mbeya kwa sababu haitaweza kuzifikia pointi ilizonazo Azam ambayo Alhamisi ilikata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataiga mwakani.
Azam iliyo kwenye kiwango bora kwa sasa ilikata tiketi ya kucheza michuano ya kimataifa mwakani baada ya kuilaza Ruvu Shooting mabao 3-0 katika mechi ya kiporo siku ya Alhamisi na kufikisha jumla ya pointi 56, akisaliwa na pointi tatu tu za kutangazwa mabingwa.
Klabu hiyo kama itaishinda Mbeya itafikisha pointi 59 ambazo haziwezi kufikia hata na Yanga wanaowapumulia kwa mbali na pia itaweka rekodi ya kutwaa taji hilo bila kupoteza mechi yoyote kama  ilivyowahi kufanya Simba mwaka 2011.
Yanga inayopo nafasi ya pili na pointi 52 kufuatia kuilaza Kagera Sugar kwa mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa siku ya Jumatano, itakuwa jijini Arusha kuomba wapete ushindi na pia kuiombea mabaya Azam mjini Mbeya ili wasubiri mechi za kufungia msimu kujua hatma yao.
Mbali na mechi hizo mbili ambazo ndizo zinazoangaliwa sana kwa sababu ya nafasi yake ya kutoa bingwa mpya wa msimu wa 2013-2014, pia leo kutakuwa na mechji nyingine mbili Simba iktakuwa uwanja wa Taifa kuikaribisha Ashanti Utd na Mgambo kuialika Kagera.
Simba itakuwa ikitaka kulinda heshima yake tu mbele ya Ashanti inayopigana kuepuka kushuka daraja kwa sababu hata ikishinda haiwezi hata kuingia kwenye Tatu Bora.
Vijana wa Msimbazi wanaonolewa na Zdrakov Logarusic yenyewe ina pointi 37 na kama itashinda mechi hiyo na ile ya watani zao Yanga itafikisha pointi 43 ambazo zimeshapitwa na wapinzani wao wa juu.
Hata hivyo Ashanti imeapa kuitoa nishai 'Mnyama' ili kufikisha pointi ambazo zitawanusuru kushuka daraja ikiwa ni msimu wao wa kwanza tangu warejee kwenye ligi hiyo, huku Mkwakwani Tanga Mgambo nayo itakuwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Kagera.
Timu hiyo nayo ipo kwenye janga la kushuka daraja, japo nafasi yake ya kusalia kwa msimu ujao ni kubwa kutokana na rekodi yao ya kushinda mfululizo kwenye duru la pili ikiwa imezitungua Simba, Yanga na Coastal Union.
Msimamo Top 4
                                  P    W     D     L     F    A    GD  PTS
01.Azam                    24   16    08   00   48   14   34   56
02.Yanga                   24   15    07   02   58   17   41   52
03.Mbeya City          24   12    10   02   30   17   13   46
04.Simba                  24   09    10   05   40   25   15   37

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...