Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, April 14, 2014

Kocha Azam kicheko kitupu baada ya ubingwa


Kocha Joseph Omog (kushoto) toka Cameroon akiwa na msaidizi wake
KOCHA Mcameroon, Joseph Marius Omog amefurahia ushindi wa jana wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji Mbeya City Uwanja wa Sokoine ulioihakikishia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara timu yake, Azam FC, lakini amewaambia wachezaji wake, pati ni baada ya mechi ya mwisho Aprili 19, mwaka huu.

“Ni furaha sana, tumepambana sana, haikuwa kazi nyepesi, tumepitia mechi ngumu tangu naanza kazi hapa, lakini tulibaki kwenye dhamira yetu na tukaendelea kupambana hatimaye tumetimiza malengo. Sote tuna furaha sasa, kila mtu ana sababu ya kufurahia kazi yake kati yetu,”alisema Omog.

Omog amewataka wachezaji wake kutobweteka na matokeo ya jana, na badala yake waelekeze nguvu zao katika mchezo wa Aprili 19, ili washinde na kukabidhiwa Kombe kwa furaha. 

“Nasikia Yanga walikata rufaa, hata kama haina maana, lakini lazima tushinde mechi ya mwisho, wachezaji wangu wanajua hilo, nimewaambia,”alisema.

Mabao ya Gaudence Mwaikimba na John Bocco ‘Adebayor’ kila kipindi jana yalitosha kuihakikishia Azam FC ubingwa wa Ligi Kuu Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya dhidi ya bao la Mwagane Yeya.

Ushindi huo, umeifanya Azam ifikishe pointi 59 ikiwa na mchezo mmoja mkononi ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote baada ya mechi za mwisho Aprili 19, mwaka huu.

Nafasi ya pili tayari ni Yanga SC yenye pointi 55 sasa baada ya jana kuifunga JKT Oljoro 2-1 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha ambayo kama itawafunga pia na Simba SC wiki ijayo itafikisha pointi 58, ambazo haziwezi pia kufikiwa na timu za chini
yake.

Azam FC itacheza mechi ya mwisho nyumbani, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam Jumamosi wiki hii, dhidi ya JKT Ruvu ikiwa na dhamira ya kushinda ili kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu bila kupoteza mechi.

Kikosi cha Azam kinaondoka leo Saa 10:00 mjini Mbeya kwa ndege kurejea Dar es Salaam na wachezaji watapewa mapumziko ya siku moja kabla ya kukutana kwa maandalizi ya mchezo wa kufungia pazia la msimu. 

LIWAZO ZITO

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...