![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj4uz3_nenRaMnOKV7SkLWXYwWmQRNBH4t6YoRC2_m1MVo22ASszqSxkCBeLloofdtc_4YVHIB4n0EeeX15NrWZj38dDPomKLvv3ZRUpw0-d1oTluwbh4l0E5yl3JpP1rBARit-fQ5QOPA/s1600/2.Kinana+akihutubia+wananchi+wa+Kijiji+cha+Lwampembe%252C+Nkasi.jpg)
Katika safari iliyomchukua zaidi ya saa tisa, Kinana na msafara wake
alikumbana na changamoto kubwa ya ubovu wa barabara kutoka Namanyere
hadi kwenye vijiji vya kata hiyo kutona na magari kunasa mara kwa mara
kwenye tope na makorogoro kwa kuwa barabara haijapata kufanyiwa
matengenezo kwa muda mrefu.
Kufuatia kujionea changamoto hiyo, Kinana amewambia wananchi wa vijiji
vya Wampembe na Ntemba, kuwa ataishauri serikali kuifanya barabara hiyo
iwe chini ya Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) badala ya sasa ambapo
ipo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na hivyo kuwa vigumu
kupatikana fedha za kutosha kujenga barabara hiyo.
Pichani
Kinana akizungumza na wananchi katika kijiji cha Wampembe, jana,Aprili
Mosi, 2014. Na zinazoendelea ni picha zaidi za ziara hiyo na changamoto
hizo alizokumbana nazo kama zilizvyopigwa na Bashir Nkoromo aliyeko
kwenye ziara hiyo.
Kinana akizungumza katika mkutano wa hadhara aliofanya katika Kijiji cha Wampembe, wilayani Nkasi mkoani Rukwa
Wananchi wa Kijiji cha Wampembe wakijimwayamwaya kwenye mkutano wao na Kinana
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhruQupWZpHDVfHCybABXGAglqu1616ZPQpiwwP7SRu4Wekz6cf8T03K5-AsortCrmgkZr0nubKPdZcVawgkzo3KzSUMDD7dRcbalWm0d40eohd_27KR-K8_4Jqp7Tg5CaNYOUIZiYVdKM/s1600/4.+Kinana+akikagua+ujenzi+wa+Kituo+Cha+Afya+cha+Wampembe+wilayani+Nkasi+mkoani+Rukwa.+Kulia+ni+Mgaga+Mkuu+wa+Kituo+hicho%252C+Dk.+Mwabulambo+Gwamaka.jpg)
Kinana
akikagua ujenzi wa Kituo Cha Afya cha Wampembe wilayani Nkasi mkoani
Rukwa. Nyuma yake ni Mgaga Mkuu wa Kituo hicho, Dk. Mwabulambo Gwamaka
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhyL4YZrxtTW71YDkGo1FY2pfvY4MIf2cqao8y16filTAZJfKne2xNKH7w4SxdM_7gDVXcGVyZCHU9-VTYz9UPhOxogXuY7PcnZN_zumtKDAA1TIGaIrLbrrVISVZ9f64wcf1AQNvfzS1c/s1600/6.+Kinana+akiwafurahia+vijana+aliowakuta+wakifanya+kazi+katika+kijiji+cha+Wampembe+kilichopo+kilometa+100+kutoka+Nkasi+mjini..jpg)
Kinana mama, baba na watoto wakimpokea kwa hamasa kubwa Kinana katika kijiji cha Wampembe
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgHm2LljlSq7zUrOyacVcn9SFAVCv-1PiCkwaQCAGn0CE7fAXcBrRLeS8dr8nL59v5ZnetJ2tN4mf4-i7ZhY9NuOA5BbVgB8Xugf7IOAb0B2esDuNzGRHcFwz4OJnMqig9u4vHrEBqjU-Y/s1600/8.+Kinana+akizungumza+na+wananchi+saa+mbili+usiku%252C+baada+ya+kuzuia+msafara+wake+eneo+la++kijiji+cha+Ntemba+kaya+ya+Kate+akitoka+Kata+ya+Wampemba+kwenda+Sumbawanga+mjini+leo.jpg)
Wananchi
katika kijiji cha Ntemba Kata ya Kate wilayani Nkasi wakimsikiliza
Kinana, alipoamua kuzunguza nao baada ya kumzuia njiani akitoka Wapembe
kwenda Sumbawanga
CHANGAMOTO ZA BARABARA
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLFhUZjdzvSFcxz9uGqVJxRIyjd_v646nrlERZdU25iVSz-e8tUR9RvJNCXgwiWd5-4NeoFuB9asmlL2o9GzT4vLg03TU3HKDBltEGhYax9mC7ZHPxvfRRZr4AuOV39V8-_zTBlURrRlQ/s1600/10.+Kinana+akishiriki+kuweka+mawe+kuweza+magari+kupita%252C+baada+ya+magari+ya+msafara+wake+kunasa+kwenye+pori+la+akiba+la++Nkasi%252C+wakati+Kata+ya+Wampembe.jpg)
Kinana
akishiriki kuweka mawe kuweza magari kupita, baada ya magari ya msafara
wake kunasa kwenye pori la akiba la Nkasi, wakati akitoka Kata ya
Wampembe
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj5e1uStgpcXJAXit7MEBnZk4kQI0zJxg4jpt8dKmkkwAxzBVoWPlHiLPugauzgbS6lJIh4DN4SGpmDGiKye-TCPOwWAxVYtOmEgrKacaieoNrDvnaA85KOwewfT6rZen6F35kcM_BP0Xo/s1600/12.+Kinana+akitazama+moja+ya+gari+la+msafara+wake++ambalo+lilinasa+porini+wakati+dereva+akijaribu+kukwepa++eneo+baya+kwenye+pori+la+akiba+la++Nkasi%252C+wakati+akienda+Kata+ya+Wampembe.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgoLLlP88IAU9iulb_S93cn0Il5zpOmA89bJYIR0fYDF_pKu8Z7eLTOgHpqO9mGRx08shwlzZxxdSWw9HnM2ezh4pquNgp0ugnSr1utkWvlK8CfQMZKIdaTjk89TjyT86ySFJKza6XvGtY/s1600/14.+Gari+la+polisi+waliokuwa+wakisindikiza+msafara+wa+kinana+likisukumwa+baada+ya+kukwama+katika+barabara+ya+kutoka+Wampemba+kwenda+Namanyere+wilayani+Nkasi.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgUr2g3UW15etKw8pDzfxHGRSwjWNvbeDVGk5HVJbkgaQOTA6-hOx-Xf-lcnvVXBcq8XWBBHym2EfaYkkowmzKTOctvAS-08t_Hkejv9LDy98VxuuZoosg4a2sWSuOWm3cIKNxS9eKZCow/s1600/16.+Kinana+na+Mwenyekiti+wa+CCM+mkoa+wa+Rukwa+wakitazama+barabara+ya+kwenda+kata+ya+Wampembe+kutoka+makao+makuu+ya+wilaya+ya+Nkasi.jpg)
MTI WA NGUVU ZA KIUME
Waandishi
wa habari kwenye msafara wa Kinana akishangaa mti ambao unakarinia
kuanguka kutokana na kumegwa vbanzi na watu wanaoamini kwa vibanzi
kutoka mti huo ni dawa ya nguvu za kiume. mti huo upo pembeni mwa
barabara ambako magari ya msafara wa Kinana yalinasa wakati wa kwenda na
kutoka kijiji cha Wampembe.
Jamaa akigema kibanzi kwenye mti huo.
No comments:
Post a Comment