Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, April 10, 2014

Azam yakata tiketi ya CAF, Ruvu kumbe debe tupu!


Azam ilipokuwa ikishiriki Kombe la Shirikisho kwa mara ya kwanza mwaka jana
KLABU ya soka ya Azam imekuwa klabu ya kwanza kukata tiketi ya michuano ya CAF baada ya jioni yua leo kuifumua timu ya Ruvu Shooting kwa mabao 3-0 na kubakisha hatua chache kutwaa taji la Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mabao ya kipindi cha kwanza yaliyowekwa kimiani na Gaudence Mwaikimba katika dakika ya 8 kwa kichwa na jingine na dakika ya 37 kupitia Himid Mao, yaliifanya Azam iende mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.
Mu Ivory Coast, Kipre Tchetche akipigilia msumari wa mwisho sekunde chache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili katika jeneza la Ruvu iliyokuwa imetamba kuwa ya kwanza kuwatungua Azam ambayo imecheza mechi 24 bila kupotea hata mchezo mmoja baada ya kufunga bao la tatu.
Kwa ushindi huo Azam imefikisha pointi 56 ambazo haziwezi kufikiwa na klabu yoyote ya Ligi Kuu zaidi ya Yanga waliopo nafasi ya pili na pointi 52.
Ushindi huo pia, umeifanya timu hiyo kukaribia kutwaa taji hilo kwani imesaliwa na mechi moja tu kati ya mbili kuweza kutangazwa kuwa bingwa kwa mara ya kwanza katika ligi hiyo na piaa kuweza kukata tiketi ya Ligi ya Mabingwa baada ya kuiwakilisha mara Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Uhakika wa Azam kuwa bingwa au la itafahamika Jumapili watakapoifuata Mbeya City kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya wakati Yanga watakaribishwa na Oljoro JKT jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...