Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, May 16, 2014

AMINA NGALUMA AFARIKI DUNIA NCHINI THAILAND AKIFANYIWA UPASUAJI WA KICHWA


Aliyewahi kuwa mwanamuziki wa dansi wa bendi za African Revolution 'Wana tam tam' na Double M, enzi hizo chini ya uongozi wa Muumin Mwinjuma, Amina Ngalum A.K.A Japanese (pichani enzi za uhai wake) amefariki dunia nchini Thailand, ambako alikuwa akifanya shughuli zake za kimuziki.

Akizungumza na mtandao huu, mtoaji wa habari hizi, aliyewahi kuwa Mkurugenzi wake katika bendi ya Tam Tam, Asha Baraka, amesema kuwa Amina amefariki dunia wakati akifanyiwa upasuaji.

''Imeelezwa kuwa Amina alianza kuugua ghafla, huku akilalamika kuwa kichwa kinamuuna na tumbo, na ndipo alipokwenda hospitali kwa ajili ya kupima na kuambiwa kua alikuwa na uvimbe kichwani na hivyo kutakiwa kufanyiwa upasuaji,

Aidha ilielezwa kuwa uvimbe huo ulikuwa ukitoa damu na baada ya kuanza kufanyiwa upasuaji hakuweza kuamka tena na ndipo umauti ulipomfika''. alisema Asha Baraka.

Mpaka mauti yanamfika, Amina alikuwa mwanamuziki wa bendi ya Jambo Survivors. Msiba upo Kipunguni B, Machimbo jijini Dar es Salaam. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU AMINA MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...