Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, May 21, 2014

WASANII WA MUZIKI WATARAJIA KUSHIRIKI SHEREHE ZA FIESTA CONGO


 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akizungumza na ujembe wa watu kutoka Congo hawapo pichani waliomtembelea ofisini kwake kuwaalika wasanii kutoka Tanzania kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo kwa lengo la kudumisha amani na mshikamano katika nchi za maziwa makuu. Kulia ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akifafanua jambo kwa wajumbe wa maandalizi ya fiesta kutoka Congo walipomtembelea ofisini kwake, kulia ni mratibu wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bw. Faso Mushigo Celestin na katikati ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara wapili kushoto akipokea zawadi kutoka kwa wajumbe kutoka Congo waliokuja nchini kuwaalika wasanii wa Tanzania kushiriki fiesta nchini Congo, kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko.
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiangalia CD iliyorekodiwa matukio mbalimbali ya fiesta ya mwaka jana ilivyokuwa nchini Congo. Kulia ni Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga.
Picha na: Genofeva Matemu – Afisa Mawasiliano Serikalini WHVUM
Na: Genofeva Matemu 
Wasanii wa muziki nchini waalikwa kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo zinazotarajiwa kufanyika julai 16 hadi 26 mwaka huu.
Mwaliko huo umetolea na wajumbe kutoka Congo walioshiriki katika siku ya Uanuwai wa Utamaduni duniani iliyoadhimishwa kitaifa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo jijini Dar es Salaam na baadaye kumtembelea Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt Fenella Mukangala  ofisini kwake ambapo walimuomba wasanii wa muziki kutoka Tanzania kushiriki sherehe fiesta zitakazofanyika nchini Congo mwaka huu.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na sherehe hizo Mwenyekiti wa sherehe za fiesta kutoka Congo Bi. Anne Gizenga amesema kuwa lengo la sherehe za fiesta mwaka huu ni kuwakutanisha wasanii wa Afrika wanaoishi nchi za maziwa makuu ili waweza kupata nafasi ya kupanda mti wa amani ikiwa na lengo la kuziwezesha nchi hizo kuwa na mazungumzo ya amani.
Bi. Gizenga amesema kuwa wanatarajia kupata wasanii wa muziki kutoka nchini Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi pamoja na wasanii wa Congo watakaoshiriki fiesta ndani ya mikoa miwili nchini Congo katika mkoa wa Kivu ya Kaskazini Goma pamoja na Kivu ya Kusini Bukavu.
“Tumezunguka nchi zilizopo katika maziwa makuu tukiwaomba wasanii wa nchi hizo kushiriki katika sherehe za fiesta nchini Congo ambazo mwaka huu tutahusisha upandaji wa mti wa amani tukizitaka nchi hizo ziwe na mazungumzo ya amani na mshikamano” alisema Bi. Gizenga.
Kwa upande wake waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara amewashukuru wajumbe hao kwa mwaliko na kuwahaidi kuwa wasanii kutoka nchini Tanzania watapata fursa ya kipekee hivo ni muhimu kwao kushiriki ili waweze kuiwakilisha Tanzania na kuweza kupata uzoefu kutoka nchi jirani.
Aidha Dkt. Mukangara amesema kuwa ni muhimu kwa Tanzania kushiriki katika sherehe hizo kwani Tanzania ilishiriki kwa kiasi kikubwa katika kuleta amani ya nchi ya Congo hivyo aina budi kushiriki na kuendeleza amani na mshikamano wa nchi hizo mbili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...