Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, May 20, 2014

WASHINDI WA MAISHA PLUS NA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2014 WAPATIKANA NA KUONDOKA NA MILIONI 50

Bahati Muriga mshindi wa Mama Shujaa wa Chakula 2014 akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Tzshs. Milioni 25 aliyoshinda kwa ajili ya vifaa vya kilimo. Kutoka kulia ni Babu wa kijiji, Epheta Msiga wa DMB na Mkamiti Mgawe kutoka Oxfam.
Mshiriki Boniphace Meng'anyi Nyakena akipokea mfano wa hundi ya Tzshs. Milioni 25 alizoshinda katika msimu huu. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Jane Foster, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Yamungu Kuyandabila, Babu wa kijiji, mwakilishi kutoka Datavision International pamoja na Epheta Msiga ambaye ni afisa mradi wa Maisha Plus kutoka kampuni ya DMB.
 Mkurugenzi Mtendaji wa DMB ambao pia ni waandaaji wa shindano la Maisha Plus Masoud Ally (Kipanya) akiwa anatoa Miongozo mbalimbali wakati wa Sherehe hizo za kumpata mshindi wa Maisha Plus Na mama Shujaa wa Chakula 2014
Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akitoa Hotuba yake wakati wa Fainali za kumpata mshindi wa Maisha Plus na Mama shujaa wa Chakula 2014
Mgeni  Rasmi katika Fainali za kumpata Mshindi wa Mama Shujaa wa Chakula na Maisha Plus 2014 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Yamungu Kuyandabila  akitoa hotuba yake.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...