Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, May 12, 2014

MANJI: NITASAJILI WACHEZAJI WAKALI , MTAWASAHAU DOMAYO NA KAVUMBAGU, UWANJA WA KISASA LAZIMA NIJENGE PIA


 SAM_1702Na Mwandishi wetu

Mwenyekiti wa Young Africans Bw Yusuf Manji amesema kuondoka kwa wachezaji wao wawili Didier Kavumbagu na Frank Domayo sio mwisho wa timu ya Yanga, kwani uongozi wake unaendelea na mipango ya kuhakikisha inasajli wachezaji wengine wazuri ambao wataisadia timu kwenye msimu ujao kwa kufuata maelekezo ya Benchi la Ufundi.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu leo, Manji amesema yameongelewa mengi sana kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao hakuwepo nchini kwa ajili ya kazi zake binafsi lakini sasa amerejea na maandalizi ya msimu ujao yameshaanza.
Kuondoka kwa Kavumbagu ni kutokana na kuchelewa kwa majibu ya TFF juu ya idadi ya wachezaji wageni kwa msimu mpya, huku Domayo ambae tangu mwaka jana aliombwa kuongeza mkataba alikua akisema anamsubiria mjomba wake ndipo aweze kufanya hivyo.
Pamoja na kuondoka kwa wachezaji hao bado kwa kushirikiana na kocha Hans watahakikisha Yanga inaendelea kutisha msimu ujao na kufanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa, Hans aliahidi kuleta wachezaji wazuri watakaoisaidia Yanga siku alipokua akiiongea na waandishi wa habari kuwaaga.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...