Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, July 3, 2013

Wasanii Tamasha la Filamu Grand Malt watoa msaada jijini Mwanza


Picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.
Sehemu ya vyandarua vilivyotolewa msaada vikiwa tayari vimefungwa na wasanii wa filamu hapa nchini,mara baada ya kutoa msaada wa vyandarua hivyo ndani ya wodi ya wazazi kwenye hospitali ya Mkoa wa jiji la Mwanza-Sekou-toure mapema leo asubuhi kwa udhamini mkubwa wa kinywaji kisicho na kilevi cha Grandmalt.

Na Mwandishi Wetu, Mwanza
WASANII maarufu wa Bongo Movie hapa nchini, ambao wapo hapa kwa ajili ya Tamasha la Wazi la Filamu Tanzania, maarufu kama ‘Grand Malt Tanzania Open Film Festival’ jana walikabidhi vyandarua kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Sekou Toure.
Akizungumza na wasanii hao, Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Halifa Hassan Hida, aliwashukuru wasanii hao kwa msaada huo na kuwataka wawasaidie pia wasanii wachanga wa jijini hapa ili nao waweze kutoka.

“Nimefarijika na msaada huu pamoja na ujio wenu, ila kimoja ninachokiomba kutoka kwenu ni kuwasaidia wasanii wa Mwanza ili nao waweze kutoka, naamini ujio wenu ni changamoto kubwa kwao,” alisema Hida.
Kaimu Meya wa Jiji la Mwanza, Dismas Masuni naye alitoa shukrani kwa msaada huo na kusema wapo ni vema zaidi kwa wasanii hao pia kufikiria kuwekeza jijini hapa kwa ajili ya maendeleo yao.
Meneja wa kinyawaji cha Grand Malt, Consolata Adam, alisema nia kubwa ya kuamua kudhamini tamasha hilo ni kuwaendeleza zaidi vijana kwani wengi wako katika ajira hiyo na kutaka wakazi wa Mwanza kufika kwa wingi wakati wote wa tamasha hilo.
Wakati walipokabidhi msaada wa vyandarua katika hospitali ya rufaa ya Sekou Toure na kuvifunga katika wadi ya wazazi, wasanii hao walionekana kuguswa zaidi na hali ilivyo na kusema wana jukumu kubwa la kuisaidia jamii. Katibu wa Afya wa hospitali hiyo, aliye pia kaimu Katibu wa Afya wa Mkoa, Danny Temba alishukuru kwa msaada huo na kusema umekuja wakati muafaka kutokana na mahitaji yaliyopo.
“Tunashukuru mno kwa msaada wenu na kwa kutaka kuwadhihirishia tuna mahitaji makubwa na vyandarua hasa katika kupambana na malaria, naomba mkavifunge wenyewe,” alisema Temba, ombi lililoridhiwa na wasanii hao na kuomba wavifunge katika wadi ya mzazi na mtoto.
Wasanii walionekana kuguswa zaidi walipoingia katika wadi hiyo, huku Jacqueline Wolper, Shamsa Ford, Chuchu Hans, Aunty Ezekiel, Vicent Kigosi ‘Ray’, Hashim Kambi na wengineo wakionekana kuguswa zaidi na mahitaji ya wadi hiyo.
“Kuna mahitaji makubwa katika hospitali hii, kuna kitu kimenigusa mno kwa kuja hapa,” alisema Jacob Steven ‘JB’, huku akiungwa mkono na Single Mtambalike ‘Ritchie Ritchie’ na Steve Nyerere.
Mratibu wa Tamasha hilo, Musa Kissoky, ambalo lilizinduliwa rasmi jana katika Uwanja wa Nyamagana alisema, kutakuwa na filamu za aina mbalimbali zitakazoonyeshwa wakati wote wa tamasha hilo.
Kissoky alisema, tamasha hilo ambalo litakuwa la bure kwa watu wote na kushirikisha mastaa wa filamu hapa nchini, litakuwa la aina yake na kuwataka wakazi wa Mwanza wajitokeze kwa wingi kushuhudia mambo yanayoendelea.
Meneja wa kinywaji cha Grand Malt walio wadhamini wakuu wa tamasha hilo, Consolata Adam, alisema wameamua kufanya kweli zaidi kwani wanataka kuona Watanzania wanapata kitu chenye uhakika. “Tumejipanga katika hili na wala hatutanii. Tunawakaribisha watu wote wenye mapenzi na filamu zetu za Tanzania kufika na kushuhudia tamasha hili ambalo mwaka huu limeboreshwa zaidi,” alisema Consolata.
Tamasha hilo la filamu limedhaminiwa na kinywaji cha Grand Malt kisicho na kilevi ambacho kinazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
Msanii wa Bongo Movie,Jacline Wolper akiwa katika wodi ya wazazi ,Hospital ya Mkoa wa Mwanza Sekou-toure akifunga chandarua kwenye moja ya vitanda hospitalini hapo,ikiwa ni sehemu ya vyandarua vilivyotolewa na wasanii hao kupitia kinywaji cha Grandmalt
Wasanii Irine Uwoya na Shamsa Ford wakiwa na mmoja wazazi akiwa amembeba mtoto aliezaliwa kwenye hospitali hiyo ya Mkoa wa Mwanza, Sekou-toure mara baada ya wasanii hao kutembelea Hospitali hiyo na kutoa vyandarua kwenye wodi Wazazi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza,Halifa Hassan Hida akizungumza machache (mbele ya wasanii wa Bongo Movie (hawapo pichani) ikiwemo na kuwashukuru wasanii hao wa filamu kwa kitendo cha kiungwana kabisa katika suala zima la kuisaidia jamii yao inayowazunguka kwa njia moja ama nyingine na pia amewataka kuwasaidia wasanii wachanga wa jiji la Mwanza na kuwaelekeza njia sahihi za mafanikio katika tasnia hiyo ambayo kwa sasa imezidi kushika kasi siku siku.
Meneja wa kinywaji cha Grandmalt Consolata Adam akipokea mkono wa shukurani kutoka kwa katibu wa Afya hospitali ya Sekou-toure Bwa.Daniel Temba,mara baada ya kabidhi msaada wa vyandarua sanjari na wasanii mbalimbali wa filamu,makabidhiano hayo yamefanyika mapema leo kwenye hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-toure,ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuwa karibu na wananchi, kisha baadae kuonyesha kazi zao mbalimbali kwenye uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
Wasanii mbalimbali wakiongozwa na Raymond Kigosi wakikabidhi msaada wa vyandarua kwenye hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-toure, kwa katibu wa afya wa Hospitali hiyo Bwa.Daniel Temba ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuwa karibu na wananchi, kisha baadae kuonyesha kazi zao mbalimbali kwenye uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
wasanii wakiendelea na zoezi la wakikabidhi msaada wa vyandarua kwenye hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-toure kwa katibu wa afya wa Hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuwa karibu na wananchi, kisha baadae kuonyesha kazi zao mbalimbali kwenye uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
Baadhi ya wasanii wa Filamu hapa nchini a.k.a Bongo Movie Unity wakiwasili kwenye hospitali ya Sekou-toure tayari kwa kushiriki zoezi la kugawa vyandarua kwenye wodi ya wazazi kwa udhamini mkubwa wa kinywaji kisicho na kilevi cha GrandMalt mapema leo asubuhi.
Mlezi wa Bongo Movie Unity,Jacob Steven a.k.a JB a.k.a Bonge la Bwana wakisalimiana na Afisa mhausiano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza,Bwa.Joseph Mlinzi,pichani kati ni msanii wa filamu Singo Mtambalike.
Baadhi ya Wasanii hao wa Bongo Movie Unit wakitoka kwenye wodi ya Wazazi mara baada ya kukabidhi msaada wa vyandarua vilivyotolewa kwa hisani kubwa ya kinywaji kisicho na kilevi cha Grandmalt.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...