Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, July 21, 2013

Golden Bush Veterani waikwanyua Faru Dume x3


Golden Bush Veterani a.k.a 'Wazee wa Dozi' katika moja ya mechi zao
WAKALI wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani jana asubuhi wameikwanyua bila huruma, Faru Dume ya Manzese kwa kuicharaza mabao 3-1 katika pambano la kirafiki lililochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Golden Bush ilipata ushindi wake huo mnono kupitia mabao ya Waziri Mahadhi 'Mandieta', Kudra Omar na Ally Chuo yaliyotosha kuizima Faru katika pambano hilo.
Uongozi wa Golden Bush ulisema umeridhishwa na kiwango cha timu yake na kwa sasa wanaendelea kujipanga kwa ajili ya mechi nyingine za kirafiki ili kugawa 'dozi' kwa wapinzani wao watakaoshuka mbele yao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...