Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, July 30, 2013

Airtel yakabidhi milioni 14 kwa washindi wa promosheni ya Airtel yatosha.



 Mteja wa Airtel mkoani arusha bw, Robert Justin akihesabu pesa zake alizojishindia wakati wa promosheni ya Airtel yatosha mara baada ya kuzitoa kupitia njia ya Airtel Money katika ofisi za Airtel mkoani
Arusha.

 Meneja wa airte Mauzo wa kanda ya kaskazini Stephen Akyooo akikabidhi shilingi milioni 1 kwa Bw, Robert Justine wa jijini Arusha fedha alizojishindia katika promosheni  ya Airtel Yatosha inayoendeshwa na Airtel maalum kwa wateja  wake wote wanaotumia huduma ya Airtel Yatosha kwa wiki, siku au mwezi mbapo pia mteja anaweza kujishindia moja kati ya Nyumba 3 za kisasa zilizopo dar es salaam.
Meneja wa airtel kanda ya kaskazini Stephen Akyoo akiwa na washindi wawili wa shilingi milion moja wa shindano la airtel yatosha kutoka  mkoani Arusha bw, Robert Justine and Balistus Mambo. Washindi wote walikabidhiwa shilingi milioni moja kila mmoja walizojishindia katika promosheni ya Airtel yatosha na kuzitoa kwa Airtel Money.


=======  =======  =====

Airtel yakabidhi milioni 14 kwa washindi wa promosheni ya  Airtel yatosha.
•         Ni washindi wa shilingi milioni moja wa wiki ya kwanza na ya
pili ya promosheni

Jumapili 28 julai 2013, kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaa na kuwazawadia washindi 14 wa kila siku wa promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba  kila mmoja shilingi milioni moja pesa taslimu kupitia huduma ya Airtel Money.

Washindi hawa wamepatikana kupitia droo ya wiki ya kwanza na ya wiki ya pili ambapo jumla ya washindi 14 kutoka katika mikoa mbalimbali ya nchi walipatikana na hatimaye kukabithiwa pesa zao

Akiongea wakati wa kukabithi zawadi kwa washindi hao Meneja Mauzo wa
Kanda Mkoani Arusha  bwana Stephen Akyoo  alisema” leo tunayofuraha

kupata washindi wa promosheni ya Airtel yatosha na kuwakabithi zawadi zao. Washindi hawa wamepatikana kutoka katika mikoa mbalimbali na kujishindia kila mmoja shilingi milioni moja pesa taslimu kwa kutumia
huduma za Airtel yatosha  na kujiunga na vifurushi vyetu mbalimbali. nae Meneja Uhusiano wa Airtel Akitangaza majina ya washindi hao bwana
Jackson Mmbando alisema "washindi wetu wa wiki ya kwanza na ya pili ni
pamoja na  Hawa Said Mkazi wa Mtwara, John Masawe mkazi wa singida,

Joseph Emmanuel Nchimbi Songea,  Rosemary Michael na John Masanja kutoka Tabora , Zuhura Sabuni kutoka Lindi, Balistus mambo kutoka Moshi, Robert Faustine kutoka Arusha ,  Frank Ladislaus na Paulina Michael kutoka Sengerema Mwanza, Flavian Adamson Malilo kutoka Katavi,

Jacob Muhole kutoka Dodoma,  Singodi Severin kutoka Kagera  na Ephrasia Thadeo kutoka Ngara.

Ili kushiriki mteja anatakiwa kupiga  kupiga *149*99#  na kununua kifurushi cha huduma ya Airtel yatosha cha siku, wiki au mwezi na kuunganishwa mojakwamoja kushiriki kwenye promosheni na kupata nafasi ya kushinda nyumba au pesa taslimu shilingi milioni moja kila siku.

Akiongea mara baada ya kukabithiwa zawadi hiyo Bwana Robert Justine moja kati ya washindi anayetokea mkoani Arusha alisema” nimefurahi

sana kuwa mshindi wa promosheni na ntaendelea kutumia huduma ya Airtel
yatosha ili kuendelea kufaidika na huduma hii na kupata nafasi ya
kushinda nyumba. Natoa wito kwa watanzania kutumia huduma hii na
kuhakikishia   hata wao wananafasi ya kushinda kama mimi nilivyoweza

leo kukabithiwa shilingi milioni moja kwa kutumia tu huduma ya Airtel
yatosha. Promosheni ya Airtel yatosha bado inaendelea kwa mienzi mitatu hadi hapo mwishoni mwa mwenzi wa tisa ambapo mbali na zawadi za pesa taslimu wateja pia wanapata nafasi ya kujishindia nyumba 3 zilizopo kigamboni jijini Dar es saalam

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...