Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, July 8, 2013

Umoja wa Mataifa yanyakua Tuzo Maalum katika Maonyesho ya 37 ya Biasharaya Kimataifa jijini Dar



photo (26)
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Shirika la Umoja wa Mataifa kwenye maonyesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa yaliyofikia tamati jana kwenye viwanja vya Mwl. Julius Nyerere jijini Dar. Waziri Mkuu aliambatana na Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda pamoja na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic Kacou.
photo (29)
Waziri Mkuu Mizengo Pinda ( wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Wajasiriamali wanaofadhiliwa na UNIDO kwenye banda la Shirika la Umoja wa Mataifa akiwa ameambatana na Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda (kushoto) pamoja na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic Kacou (wa pili kulia) wakati wa sherehe za kufunga Maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa jijini kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.
photo (33)
Tuzo maalum waliyokabidhiwa shirika la Umoja wa Mataifa nchini kwa kutambua mchango wao wa kuhamasisha Jamii (UN Special recognition for community awareness) wakati wa sherehe za kufunga Maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...