Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 3, 2013

NHIF YAZINDUA HUDUMA ZA BIMA YA AFYA YA JAMII (CHF)MJINI KILWA 1

1Adoh Mapunda Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa akipokea vifaa maalum vya kuhifadhia fedha na nyaraka mbalimbali kutoka kwa Balozi Ali Mchumo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakati wa uzinduzi wa Huduma za Bimaya Afya (CHF)katika halmashauri hiyo uliofanyika jana kwenye viwanja vya Mkapa Garden Mjini Kilwa, wa pili kulia anayeshuhudia tukio hilo ni Kaimu Mkurugenzi wa (NHIF) Khamis Mdee na kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), Athuman Rehani na Fortunata Raymond Msimamizi wa NHIF mkoani Lindi.wananchi mbalimbali wakiwemo wazee walijitokeza katika zoezi la upimaji wa afya yakiwemo magonjwa ya Kisukari, Shinikizo la Damu ikiwani pamoja na kupima Uzito Urefu.  2Ado Mapunda Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa huduma za Bima ya Afya katika Halmashauri ya wilaya ya Kilwa jana kulia ni Bw. Khamis Mdee Kaimu Mkurugenzi NHIF na kushoto ni Dr. Hilda Mwakipesile kutoka NHIF 3Baadhi ya wazee wakisubiri kupata huduma ya upimaji wa afya zao katika viwanja vya Mkapa Garden mjini Kilwa jana 4Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Mfuko wa taifa wa Bima ya Afya NHIF Balozi Ali Mchumo akipata huduma ya vipimo kutoka kwa mmoja wa madaktari wa NHIF jana anayeshuhudia ni mama Fatma Said Ali Mke wa Balozi Ali Mchumo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...