Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, September 7, 2013

ALEX MSAMA ATEULIWA KUWA MJUMBE WA BASATA



Na Veronica Kazimoto – MAELEZO, Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Penina Mlama (pichani) kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari - MAELEZO, Uteuzi huo wa Profesa Mlama unaanzia mwaka 2013 na unatarajia kumalizika mwaka 2016.

Prof. Mlama ni Profesa wa Sanaa na Sanaa za Maonyesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Aidha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla watu 12 kuwa wajumbe wa BASATA kwa kipindi cha
miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka huu.

Walioteuliwa ni pamoja na wawakilishi wa Vyama na Asasi mbalimbali wa Baraza hilo ambao ni Dkt. Vincensia Shule, John Kitime , Angela Ngowi, Dkt. Herbert Makoye, Erick Shigongo na Alex Msama.
ALEX MSAMA

Wawakilishi wengine ni pamoja na Juma Adam Bakari, Daniel Ndagala, Michael Kadinde na Joyce Fisoo.

Wanaoingia kwa mujibu wa nyadhifa zao ni Prof. Hermas Mwansoko na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Katika hatua nyingine Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara amemteua Bwana Ghonche Materego kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). 

Kabla ya uteuzi huo Materego alikuwa amemaliza muda wake kama Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa.

Wajumbe wa Bodi hiyo walioteuliwa na Waziri Mukangara ni Dkt. Herbert Makoye, Prof. Emanuel Mbogo, Dkt. Lucy Mboma, Prof. Hermas Mwansoko pamoja na Katibu Mtendaji wa BASATA.

Wakati huo huo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla ya watu 21 kuwa wajumbe wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka 2013 hadi 2015. 

Wajumbe hao ni Dkt. Shani Omari, Prof. Yohana Msangila, Ester Riwa, Dkt. Issa Zidi, Khadija Juma na Dkt. Martha Qorro.

Wengine ni Mmanga Mjawiri, Razia Yahaya, Richard Mbaruku, Selina Lyimo, Keneth Konga, Amour Khamis, John Kiango, na Shani Kitogo. 

Wajumbe wengine ni Ally Kasinge, Ahmed Mzee, Rose Lukindo, Shabani Kisu pamoja na Edwin Mgendera.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo la BAKITA atachaguliwa na wajumbe watakapokutana kwenye kikao chao cha kwanza.

Bonanza la mazoezi la Vita Malt Arusha


ARUSHA, Tanzania

KATIKA kuhakikisha Watanzania wanakuwa na afya bora, kinywaji kisicho na kilevi cha Vita Malt, kimeandaa bonanza maalumu litakalowashirikisha wafanya mazoezi ambalo linatarajiwa kufanyika katika Viwanja vya General Tyre, jijini hapa leo.


Meneja wa Vinywaji visivyo na Vileo katika Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Consolata Adam alisema, baada ya kufanyika Dar es Salaam na Mwanza wameamua kulileta Arusha kabla ya kuelekea Mbeya.


Kuhusu bonanza la leo, Consolata alisema, anaamini litakuwa la aina yake na linatarajiwa kuanza saa 2 asubuhi na kuwataka wakazi wa Arusha kufika kwa wingi uwanjani hapo ili kufanya mazoezi kwa pamoja.


“Tumeamua kuandaa bonanza linalowakutanisha wanamichezo mbalimbali hasa wafanya mazoezi ili kuweza kukutana na kufanya mazoezi kwa pamoja.


“Katika bonanza hilo kutakuwa na gym maarufu za Arusha ambazo zitashiriki na kutakuwa na wakufunzi mbalimbali,” alisema, huku akidai mtu anatakiwa kwenda tu uwanjani kwani mazoezi hayo yatakuwa bure.


Alisema, lengo kuu kuu la bonanza  ni kuhamasisha jamii nzima kutambua umuhimu wa kufanya mazoezi ili kujenga afya bora za miili yao na pia kujenga umoja imara wa gym zilizopo nchini.


Burudani katika bonanza hilo inatarajiwa kutolewa na bendi ya Vita, huku wasanii maarufu wa Bongo Fleva wa Arusha nao wakiwepo.


“Tumeweka burudani za kila aina kwani kutakuwa na michezo mbalimbali ya kufurahisha kama soka, netiboli, kuvuta kamba, kukimbiza kuku pia na zawadi nyingi toka Vita Malt zitakuwepo.”


Naye Meneja Mawasiliano na Mahusiano wa TBL, Edith Mushi aliwataka wakazi wa Arusha kutumia fursa hii hili kufanya mazoezi kwa pamoja.


“Hii ni siku ya familia napenda kuwajulisha watanzania wote na wapenda michezo kote nchini kuwa waje mapema na familia zao.”


Vita Malt ni kinywaji kinachozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...