Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, December 26, 2013

PACQUIAO: Mbabe anayemkuna David Beckham



pacquiao na familia yake
MARA baada ya Desemba mwaka jana kupoteza pambano lake dhidi ya mbabe Juan Manuel Marquez kwa ‘KO’ mbabe na mbunge Manny Pacquiao alionekana kama zama za utawala wake katika masumbwi zilikuwa zimefikia ukomo.
Mbabe huyo amefuta wale waliokuwa na dhana hiyo baada ya kurejesha heshima yake kwa kumchakaza kwa pointi Brandon Rios mjini Macau, katika pambano alilolifanya kwa ajili ya kusaidi waathirika wa mafuriko yaliyotokea nyumbani kwao Ufilipino na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 4000 na wengine milioni nne wakikosa makazi.
Alishinda kwa jumla ya pointi 120 kwa 109 na baada ya kumalizika kwa pambano hilo Pacquiao alitamka bayana kwamba yuko tayari kupambana na bondia yeyote akiwamo mbabe asiyepigika Floyd Mayweather.
Bob Arum ambaye ni promota wa Pacquiao ametenga kiasi cha dola milioni 300 kwa ajili ya pambano hilo lakini Mayweather ameshalitolea nje kwa kusema kuwa “sina mpango wa kufanya kazi na promota huyo, kwa sababu ni mbabaishaji amekuwa akikataa kuweka pambano hilo katika miezi ninayotaka ya May na Septemba,”.
USICHOKIJUA
Usichokijua ni kwamba mwanasoka maarufu kutoka Uingereza, David Beckham amebainisha kwamba ni shabiki mkubwa wa mbabe Manny Pacquiao na kwa kuthibitisha hilo hata katika pambano lake lililopita alisafiri hadi Macau kwenda kumshangilia.
Jambo jingine ni kwamba Manny Pacquiao amekuwa ni mpenzi wa hayati Bruce Lee na amekuwa akipenda kuuweka mwili wake kama mpambanaji huyo wa zamani aliyejipatia sifa kubwa duniani.
Kuingia katika katika medani za siasa haikuwashangaza sana Wananchi wa Ufilipino kwa kuwa alishaanza kukuzwa na rais wan chi hiyo, Arroya.
Mwaka 2012, Pacquiao aliweka rekodi ya kushika nafasi ya pili ya kuwa mwanamichezo na bondia anayelipwa zaidi duniani akilipwa dola milioni 62 huku nafasi ya kwanza ikikamatwa Floyd ‘Money’ Mayweather.
Ukiachilia masuala ya ngumi pia ni mwigizaji mzuri wa filamu akiwa amecheza tamthilia kadhaa zinazoratibiwa na ABS-CBN
UTAJIRI
Mbabe huyo anamiliki utajiri unaofikia kiasi cha dola milioni 100 (sawa na shilingi bil. 160).
Fedha hizo amekuwa akiziingiza kwa mchezo wa ngumi na kufanya matangazo mbalimbali ya kibiashara ikiwamo tangazo la bia za San Migue.
Ukiachilia hayo mbabe Manny anamiliki baada yake kubwa katika maeneo maarufu kwa starehe katika kisiwa Boracay huko Aklan akiwa ameshirikiana na mfanyabiashara mwingine, Crisostomo ‘Cris’ Aquino waliyoianzisha tangu mwaka 2006.
Baa ya wawili hawa inajulikana kwa jina la Boracay West Cove ikiwa

Manny Pacquiao Decided to Still Continue Boxing Career Despite Wife’s Plea

Manny Pacquiao was shockingly knocked out in his fight with Juan Manuel Marquez but that does not stop the Filipino boxing champ.

According to Pacquiao, he still wants to continue boxing even though his wife Jinkee requested him to retire now.

The 33-year-old Filipino boxer fell down face first on the canvas from a knock-out punch then remained unconscious for several seconds as his wife tried to enter the ring. Jinkee Pacquiao admitted that she was terrified after witnessing what happened to her husband causing her to scream and cry before promoter Bob Arum calmed her down.

"It's the first time I've seen him like that, lying on the canvas, and I was scared,'' Jinkee Pacquiao told USA TODAY Sports. "I know he is still capable of fighting but for me there is nothing to prove. He already has eight title belts. He can retire - stop - at anytime. I want him to stop now. But he is the one who has the last say. Boxers risk their lives, some end up in wheelchairs. I don't want that to happen to Manny," Jinkee further stated.

Manny Pacquiao confirmed to USA TODAY Sports that he has no intentions of retiring after his loss to Juan Manuel Marquez.

"I remember hitting the canvas. My head dropped - boom! But I feel good. He just got lucky with that one punch. It made good impact because my face was going forward. It was all timing. He threw the punch without looking and he was surprised it landed. But give him credit," Pacquiao stated.

One significant basis why Manny Pacquiao wants to continue fighting is his finances. "Pacquiao has already earned huge sums of money in the last three years which includes an estimated gross of $175 million in the ring," Bob Arum revealed to USA TODAY Sports.

The couple reportedly has an extravagant money spending habits aside from the donations given to charitable causes. Mike Koncz, business adviser and chief negotiator of Manny Pacquiao, is now a little bit concerned over the couple's unnecessary lifestyle.

"Sometimes Manny gets angry with me because I'm overprotective of his money," Koncz revealed to USA TODAY Sports.

"In a general sense, we're not in the position to sustain the same lifestyle now if he were to stop fighting tomorrow. He could quit tomorrow and live comfortably. Could he quit tomorrow and live extravagantly like we are now? No," Koncz further added.

Manny Pacquiao returned to the Philippines where his family and friends gave him a warm welcome. He will celebrate his 34th birthday on December 17 then go on a come back holiday trip to Israel with several family members from December 19-30.
inakarabatiwa kila mwaka kwa kufanya kuwa na muonekano mzuri na mpya.
NYUMBA
Mbabe huyo anamiliki mjengo mkubwa nchini mwao, ikiwa na vyumba vya kulala saba, nyumba hiyo iko kwenye eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 2,300.
Paa lake limejengwa kwa vigae maalum kutoka nchini Japan ikiwa ni pamoja na geti la kufunguliwa kwa rimoti.
Jumba hilo lina bwawa la kuogelea ambalo lina sura ya glovu ya ngumi, kwa pembeni ya bwawa hilo kuna vitu kwa ajili ya waogeleaji na wageni wa nyumba hiyo. Jumba hilo pia lina gereji yenye uwezo wa kuhifadhi magari saba.
Bondia huyo ametumia gharama kubwa za fedha kwa ajili ya kulifanyia ukarabati jumba hilo na kuliwezesha kuwa na muonekano mzuri na wa kuvutia.
USAFIRI
Pamoja na kwamba mbabe huyo amekuwa na magari mengi lakini amekuwa akipenda zaidi kutumia gari aina ya Brand-new Ferrari 458 Italia.
MAHUSIANO
Jinkee Pacquiao 2006, Ara Mina aliyekuwa naye tangu mwaka 2007 na Krista Ranilo aliyedumu naye tangu mwaka 2009 hadi 2010.
Mbabe huyo anaishi na mkewe anayejulikana kama Maria Geraldine Jamora na wamefanikiwa kupata watoto wanne ambao ni Emanuel, Princess, Michael na Queen Elizabeth.
WASIFU
JINA: Emanuel  Manny Pacquiao
UMRI: Desemba 17, 1978
ENEO LA KUZALIWA: Bukidnon, Mindanao, Philippines
KIMO: Futi 5 na inchi 6
UTAIFA: Ufilipino

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...