Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, February 11, 2014

NDOA YA LADY JAY DEE YAINGIA KIDUDU, AMUOMBA TARAKA GARDENER



UNAWEZA ukakataa lakini ndivyo ilivyotokea, ndoa ya mtangazaji mahiri Bongo, Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteini’ na Mbongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ iliyofungwa miaka 9 iliyopita inadaiwa kuingia kidudu kufuatia mke huyo kuomba aandikiwe talaka, ni Ijumaa Wikienda pekee lenye uthubutu wa kuripoti mkasa wote.
Jide akiwa na mmewe Gardner.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, Jide au Lady Jaydee alifikia uamuzi huo baada ya Gardner kupata kazi ya kutangazia redio moja nchini Kenya.
HABARI KAMILI
Mnyetishaji wa kisanga hiki, aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa mara baada ya mume huyo kupata mchongo mzima alirudi nyumbani akiwa na furaha na kumwambia mkewe kuhusu bahati hiyo.
“Baada ya Gardner kupata mchongo wote wa kazi alikwenda mbio nyumbani kwake Kimara (Dar) ili akamwambie mkewe.

“Pia katika safari ya kwenda Kenya kupiga mzigo ilikuwa aende na mkewe huyo kwa sababu lilikuwa suala la kuhamisha makazi yao Tanzania,” kilisema chanzo hicho.
JIDE AHAMAKI

Chanzo kikatoboa kwamba Gardner alipofika nyumbani kwake na kumweleza mkewe, alikumbana na kitu ambacho hakukitarajia.

“Komando (Jide) alihamaki na kumjia juu akisema yeye hawezi kuondoka Tanzania kwenda kuishi Kenya, kama Gardner analiona jambo hilo ni heri kwake, amuandikie talaka yake na kuachana ili kila mmoja achukue hamsini zake,” chanzo kilizidi kuporomosha maneno.
KWA NINI JIDE HAKUPENDA?
Habari zilizidi kuanikwa kwamba Jide au Binti Machozi alifikia uamuzi huo baada ya kugundua kuwa kitendo cha kwenda kuishi Kenya kitaua bendi yake ya Machozi na sehemu ya biashara ya Nyumbani Lounge iliyopo Ada-Estate, Kinondoni, Dar.
MBAYA ZAIDI

Taarifa zikazidi kumiminika kwamba, mbali na Jide au Anakonda kuhofia biashara zake kufa, lakini pia hakupenda Gardner aondoke hata peke yake kwa sababu yeye ndiye meneja wa miradi hiyo miwili.

“Mimi nilipopata habari hizo nilikutana na Jide nikamuuliza, akanijibu ameamua iwe hivyo tu, kikubwa mumewe (Gardner) aamue moja kati ya hayo mawili kwani yeye ana haki akiwa kama mkewe wa ndoa,” kilisema chanzo kikimkariri Jide.
GARDNER AISHIWA NGUVU

Kufuatia majibu ya mkewe, taarifa zinasema mtangazaji huyo ambaye alishawahi kupiga mzigo kwenye kituo cha Radio Clouds FM cha jijini Dar alijikuta akiishiwa nguvu na kuachana na dili hilo mara moja.

“Gardner alisalimu amri kwa mkewe, akaamua kuachana na dili la kwenda kutangaza Kenya. Lakini alifikiri sana akasema ni kweli kuhamia Kenya kungeua miradi yao ya Tanzania maana ingekosa msimamizi wa kuaminika,” chanzo kiliweka wazi.

KAMA ANGEKWENDA KENYA
Siri hiyo iliyovujia mikononi mwa Ijumaa Wikienda haikuishia hapo, ilizidi kuanikwa kwamba kama Kapteini angekwenda Kenya na kuanza kazi, ilikuwa alipwe mshahara wa shilingi za Kenya laki 3 kwa mwezi (kama milioni 6 za Tanzania).
NAFASI YAKE BADO IPO

Mpashaji wetu alisema kwamba nafasi ya Gardner kwenye kituo hicho cha redio ambacho hakikutajwa, bado ipo lakini tamko la Jide nalo li hai, kwa vile hakubatilisha, endapo mumewe atataka kwenda hata kesho (Jumanne) aandike talaka.
WIKIENDA NA GARDNER
Baada ya kunyetishiwa taarifa nzima, juzi gazeti hili lilimsaka Gardner. Kwa njia ya simu lilimkosa, likamfuata Nyumbani Lounge. Lilipomkuta lilimsimulia kisanga chote cha ndoa yake kutikiswa na kitendo cha yeye kupata kazi Kenya ambapo alijibu hivi:

“Ndoa ni nzuri, ni kweli ilikuwa niende Kenya, nilipata kazi kule lakini kama familia ilikuwa lazima tukae na kupanga, mwenzangu hakuafiki.”
Wikienda: “Ni kweli shemeji ameomba uchague mawili, umwandikike talaka au uende Kenya?”
Gardner: “Ndiyo maana nimesema ndoa nzuri, lazima makubaliano yawepo, mke anaweza kuonesha msimamo wake na mume kama utakaa chini na kuufikiria ukapata jibu unakubaliana na mke wako wala hakuna ubaya.”

Wikienda: “Kule mshahara wako ungekuwa shilingi ngapi?”
Gardner: “Hiyo sasa ni siri ya makubaliano.”
Wikienda: “Kwa nini usiamue kwenda tu?”
Gardner: “Nimekwambia ndoa nzuri.”
JIDE BIZE
Juhudi za kumpata Jide ziligonga mwamba baada ya muda wote kuwa bize na shoo ya kukata na shoka aliyokuwa akiifanya siku hiyo kwenye ukumbi huo akikimbiza na nyimbo zake kali za zamani na hizi mbili zilizogeuka nyimbo za taifa, Joto Hasira na Yahaya.
RAFIKI WA GADNER AMCHAMBUA JIDE

Rafiki wa karibu na Gardner (jina tunalo) ambaye alisikia mahojiano ya mtangazaji huyo na Ijumaa Wikienda, alisubiri jamaa aondoke ambapo alianza kumchambua Jide.
“Nataka kuwaambia kitu, Jide ni mwanamke jasiri sana. Ana msimamo na anaposhikilia msimamo wake hatengui hasa kama atabaini kuwa yupo sahihi.

“Ni kweli jamaa (Gardner) alipata kazi Kenya tena mshahara mzuri tu, lakini mama (Jide) akaweka ngumu hakuna kwenda,” alisema rafiki huyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...