Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 7, 2013

BATULI AWANANGA WAIGIZAJI NA MASHABIKI WANAO POST MATUSI MITANDAONI




Mwigizaji Yobnesh Yussuph maarufu kama Batuli ameamua kuwatolea uvivu waigizaji wanaoandika matusi kwenye mitandao na kuwaambia kuwa badala ya wao kupoteza muda huo kutukana matusi makali kwenye mtandao wangetumia muda huo kufanya Ibada ili wakifa waende peponi kwa Amani ambako wangeweza kupajaza mpaka wengine wakose viti.

“…Ule muda watu wanaoutumia kuandika naneno makali (MATUSI) kwenye instagram (Mtandao wa kijamii) wangekuwa wanautumia kwa ibada peponi kungejaa..” Alisema batuli.

Huku ikiwa bado haijajulikana anamlenga nani moja kwa moja na ujumbe huo baadhi ya wachunguzi wa mambo wamehusisha kauli hiyo na kitendo kilichotokea juzi cha mwanadada wa bongomovies kuporomosha matusi makali sana kwenye mtandao huo maarufu wa kijamii nchini

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...