Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 14, 2013

KINANA AAHIDI KUJENGA UPYA JENGO LA CCM LILILOTEKETEZWA VURUGU ZA GESI, PAMOJA NA KUTATUA TATIZO LA UNUNUZI WA KOROSHO


 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) akivishwa skafu ba kijana wa Green Guard, eneo la Namakongwa mpaka wa Wilaya za Tandahimba na Masasi mkoani Mtwara leo,akielekea Wilaya ya Tunduru kuanza ziara ya kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa Ilani ya CCM, katika mikoa ya Ruvuma na Mbeya.
 Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa wa CCM, Dk. Asha Rose Migiro 9kushoto) akisalimiana na baadhi ya wanachama wa CCM  ambayo yeye na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana walipolakiwa eneo la Namakongwa, Masasi leo, walipokuwa wakitokea Tandahimba  kwenda Tunduru.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akisalimiana na wanachama wa CCM wakati wa mapokezi hayo.
 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Masasi, Mtwara, wakishangilia wakati Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza nao na kuahidi kusaidia ujenzi wa Jengo la CCM la wilaya hiyo, lililounguzwa wakati wa vurugu za gezi mkoani Mtwara.
 Mkuu wa Wilaya Masasi, Kazumari Malilo akielezea mbele ya Kinana katika mkutano huo kuhusu matatizo makubwa yanaikumb wilaya hiyo kuhusu ununuzi wa zao la korosho na ujenzi wa jengo ala CCM wilaya ililoteketezwa wakati wa vurugu za gesi.
Kinana akihutubia katika mkutano huo mjini Masasi leo.PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...