Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 14, 2013

MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA NDUGU PHILIP MANGULA AMALIZA ZIARA YAKE YA KICHAMA MKOANI RUKWA


 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Hiporatus Matete wapili kushoto kwa niaba ya viongozi wa chama na Serikali Mkoa wa Rukwa akimuombea dua Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Philip Mangula wakwanza kushoto aweze kusafiri salama kuelekea Mkoani Mbeya katika maagano yaliyofanyika Mpakani mwa Mkoa wa Rukwa na Mbeya tarehe 13 Novemba 2013. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya. 
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Philip Mangula akionyesha mchoro wa asili wa Twiga aliopewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya wa pili kushoto katika hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na Mkuu huyo wa Mkoa tarehe 12 Novemba 2013 kama ishara ya kulinda na kuzipenda maliasili za taifa na kuendeleza vita dhidi ya ujangili nchini. Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Hiporatus Matete na wa kwanza kulia ni Katibu wa CCM Mkoa huo Bi. Rahel Ndengeleke.
Mhe. Mangula amesema amejifunza mengi Mkoani Rukwa ikiwemo mipango mbalimbali ya maendeleo ya Chama na Serikali, alipendezewa na maendeleo aliyoyaona sasa Mkoani Rukwa tofauti na miaka 10 iliyopita alipofika Mkoani hapo kwa mara ya mwisho. Alifurahishwa na Mpango wa Serikali ya Mkoa wa Rukwa wa ONYARU; Ondoa nyasi Rukwa ambao umehamasisha wananchi wengi kuondoa nyasi na kuezeka bati katika nyumba zao. 
 Baadhi ya viongozi wa chama (CCM) na Serikali Mkoani Rukwa wakiwa katika hafla ya chakula cha jioni cha kuagana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Ndugu Philip Mangula katika Hoteli ya Holland Mjini Sumbawanga tarehe 12 Novemba 2013.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...