Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, November 16, 2013

Kilimanjaro Stars yapangwa mchekea Chalenji Cup 2013




BARAZA la Shirikisho la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) linatarajia kutangaza ratiba rasmi ya michuano ya Kombe la Chalenji itakayofanyika nchini Kenya. tayari makundi ya michuano hiyo yametangazwa.
Tanzania Bara inayowakilishwa na Kilimanjaro Stars yenyewe imepangiwa kundi mchekea la B pamoja na timu za Zambia ambao ni waalikwa, Burundi na Somalia.
Wawakilishi wengine wa Tanzania, Zanzibar Heroes ya Zanzibar yenyewe imepangwa kundi A na wenyeji Kenya, Ethiopia na Sudan Kusini, wakati kundi la kifo ni kile la C lenye timu za Uganda ambao ni mabingwa watetezi , Rwanda, Sudan na Eritrea.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia Novemba 27 jijini Nairobi kuwania taji hilo ambalo kwa miaka mingi limetawaliwa na Waganda.
MAKUNDI YALIVYO CHALENJI 2013:
KUNDI A- Kenya, Ethiopia, Zanzibar, South Sudan

KUNDI B- Tanzania, Zambia, Burundi and Somalia

KUNDI C- Uganda, Rwanda, Sudan and Eritrea.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...