Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 21, 2013

KIKUNDI CHA NAHONDA TOTOJI MAZINGE CHA TWAA UBINGWA MBIO ZA MITUMBWI


 Mabingwa wa mbio za mitumbwi zinazodhaminiwa na bia ya Extra Lager ,kikundi cha nahodha Mhete Muhoja wakiwasili katika ufukwe wa Monarch wakati wa mbio hizo zilizofanyika mwishoni mwa wiki.
Washiriki wa mbio za mitumbwi zinazodhaminiwa na bia ya Balimi Extra Lager wanawake Ukerewe wakianza rasmi mbio hizo zilizofanyika katika Ufukwe wa Monarch Ukerewe mwishoni mwa wiki.

KIKUNDI cha Nahodha Totoji Mazinge Ngoroma kutoka Wilayani Ukerewe kimetwaa ubingwa wa mashindano ya mbio za Mitumbwi zinazodhaminiwa na Kampuni ya Bia nchini kupitia Bia ya Balimi Extra Lager na hivyo kujitwalia zawadi ya fedha taslimu Shilingi 900,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Kisiwa cha Ukerewe katika mashindano ya Kanda yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza hivi karibuni.
Nafasi ya pili ilichukuliwa na kikundi cha nahodha Toto Sebastiani ambao walizawadiwa fedha taslimu shilingi 700,000/= pamoja na nafasi ya kuwakilisha Kisiwa cha Ukerewe pia katika fainali za Kanda pale jijini Mwanza ,nafasi ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha nahodha Simon Fundi ambao walizwadiwa fedha taslimu shilingi 500,000
Upande wa Wanawake kikundi cha nahodha mwanamama Mhete Muhoja nakujitwalia ubingwa na hivyo kuzawadaiwa fedha taslimu Shilingi 700,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Kisiwa cha Ukerewe kwenye mashindano ya Kanda pale jijini Mwanza mwezi ujao. 
Nafasi ya pili upande wa wanawake ilichukuliwa na kikundi cha nahodha Jenifer Elias na ambao walijinyakuliwa zawadi ya fedha taslimu shilingi 600,000/= pamoja na kuwakilisha kisiwa kwenye fainali za Kanda upande wa Wanawake pale jijini Mwanza,nafasil ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha nahodha Edna Chambo ambao walizawadiwa fedha taslimu shilingi 400,000.
Akizungumza na wananchi waliofurika kwa wingi katika ufukwe wa Monarch Galu Beach meneja mauzo wa TBL wilaya ya Ukerewe, Josephat Changwe amesema kuwa licha ya mchezo huo kuwa burudani Kampuni yake imenuia kuyaboresha mashindano hayo ili yapate sura ya kimataifa huku yakibadili maisha ya wananchi kama sehemu ya mitaji.
Fainali za Kanda za mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Decemba 7,2013, katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza ambapo watashindana mabingwa wa Kanda nzima ambao ni kutoka Kigoma, Kagera,Ukerewe,Musoma na wenyeji Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...