Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, November 10, 2013

TAMASHA KUBWA LA EUROPEAN FILM FESTIVAL KUANZA 22.NOVEMBER 2013.


TAMASHA kubwa la filamu ambalo ufanyika kila mwaka la European Film Festival (EFF2013) lipo tayari kwa mwaka huu na litaanza rasmi tarehe 22 November 2013 kwa kuonyeshwa filamu mbalimbali katika vituo vilivyopangwa ambazo ni Alliance Francaise, Mlimani City Century Cinemax, Goethe-Institut na Nafasi ArtSpace filamu zitaonyeshwa kwa siku tatu tarehe 22, 23 na 24 November 2013.
Tamasha la hili limekusudia kuinua tasnia ya filamu ya Tanzania katika kujifunza utamaduni kutoka Ulaya katika njia ya filamu katika kuimalisha na kukuza utamaduni wan chi husika hivyo ni njia nzuri kwa watengeneza filamu wa Swahiliwood kushiriki katika kujifunza zaidi utengenezaji bora wa filamu.
Filamu nzuri na za kusismua kama vile Limbo, Kings, Tea or Electricity, The Great bear na nyinginezo zitaonyeshwa katika kujenga na kutoa nguvu sambamba na elimu burudani kutoka katika filamu husika, ni tamasha muhimu sana kushiriki kujionea tasnia kutoka Ulaya ilivyopiga hatua, KINGILIO NI BURE unaweza kutembelea www.trinitypromotionstz.blogspot.com kwa habari zaidi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...