Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 21, 2013

Paparazzi Athumani Hamis kuanza kampeni Maalum ya Usalama Barabarani


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima  akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kumtangaza  Athuman Hamisi (kulia) kuwa Balozi wa Usalama Barabarani kitaifa.

Athumani Hamisi anataraji kuanza kampeni maalum ya kuhamasisha jamii juu ya matumizi sahihi ya vyombo vya usafiri kwa kufanya kampeni hiyo kuanzia mwezi Desemba ambao umeelezwa kuwa na matukio mengi ya ajali na kusababisha vifo na ulemavu.

Pia wito umetolewa kwa wadau mbalimbali nchini na nje ya nchi ambao watapenda kusaidia jitihada hizo za Athumani Hamisi kuchangia ama moja kwa moja kwake au kupitia Kamati ya Kitaifa ya Usalama Barabarani ambayo Mwenyekiti wake ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nadani, Pereira Silima  na Katibu ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna wa Polisi, Mohamed Mpinga.  
Athumani ni Mwandishi wa habari wa shirika la Magazeti ya Serikali, Tanzania Standard Newspapers (TSN), inayochapisha magazeti ya Daily News na Habari Leo na alipata ajali ya gari huko Rufiji takribani miaka mitano iliyopita hali iliyompelekea ulemavu ambapo viungo vya mwili wake vimepooza.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...