Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 7, 2013

NIDA yaendelea kuchukua alama za kibaolojia.


 Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhifadhi Hati toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Thomas Willium akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu zoezi la uchukuaji wa alama za kibaiolojia linaloendelea katika jiji la Dar es Salaam,zoezi hili limeshakamilika katika wilaya ya Ilala na pia lipo katika hatua za mwisho katika wilaya ya Temeke na baada ya hapo litahamia wilaya ya Kinondoni,Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi.Zamaradi Kawawa.
 Meneja Mifumo ya Uchambuzi ya Kompyuta wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Bw. Mohamed Mashaka akieleza kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) utaratibu wa kuweka majina kwenye mbao za matangazo ya vituo vya usajili ili wananchi waweze kuhakiki usahihi wa majina yao.Kulia ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhifadhi Hati toka Mamlaka hiyo Bw. Thomas Willium
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhifadhi Hati wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Thomas Willium akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) kifaa cha kuchukulia alama za vidole (mobile enrolment unit).Wakati wa mkutano uliofanyia katika ukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Leo Jijini Dar es Salaam. Picha na Hassan Silayo-MAELEZO

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...