
Katika
historia yake fupi Mama huyo alifika Mkoani Rukwa kwa shughuli za
kitalii na ndipo alipomuona mtoto mmoja katika moja ya kituo cha kulelea
mayatima akiwa na hali mbaya ya kiafya huku akiwa mgojwa sana, Aliamua
kumchukua mtoto huyo na kuishi nae hadi akapona ndipo aliposhawishika na
kuamua kuhamia Tanzania na kuchukua watoto wengine yatima hadi kufikia
12 ambao kwasasa amesema wanatosha kulingana na uwezo alionao.
Aliongeza kuwa
katika kuwalea watoto hao anatumia uwezo wake yeye binafsi pamoja
na misaada mbalimbali kutoa kwa ndugu, jamaa na marafiki wa nchini
kwake Ujerumani.





No comments:
Post a Comment