Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, August 25, 2012

LAPF YAENDESHA SEMINA KWA WAHARIRI WASANIFU WA VIPINDI VYA RADIO NA TELEVISHENI MJINI MOROGORO



Meneja wa Kanda wa Mfuko wa hifadhi za wafanyakazi wa Serikali za Mitaa LAPF Bw. Sayi Lulyalya akitoa mada katika semina ya iliyokutanisha mfuko huo na Kituo cha Maendeleo cha Wahariri wa Wasanifu na Watayarishaji wa Vipindi ili kuelewesaha jinsi mfuko huo unavyofanya kazi zake na faida za kuwa mwanachama wa mfuko huo. semina hiyo imefanyika kwenye Hoteli ya Nashera mjini Morogoro.

Elias Baruti Meneja Uwezeshaji akitoa mada za uwezeshaji katika semina hiyo

Mwenyekiti wa KIMAWATA Bw. Lauden Mwabona akizungumza katika semina hiyo mara baada ya kufunguliwa rasmi wanaofuatia katika picha ni Andrew Kuyeyana Meneja Uhusiano wa LAPF, Sayi Lulyalya Meneja wa Kanda ya Mashariki LAPF na Elias Baruti Meneja Uwezeshaji.

Kutoka kulia ni Rwhema MkambaAfisa Masoko na Uhusiano LAPF, Andrew Kuyeyana Meneja Uhusiano na Elias Baruti Meneja Uwezeshaji wakijadili jambo katika semina hiyo

Mpiga picha wa Gazeti la Jambo Leo na Mmiliki wa blogu ya Kamanda wa Matukio Richard Mwaikenda akiwa pamoja na wahariri wengine katika semina hiyo

Mhariri wa Habari kutoka Clouds Joyce Shebe akiwa katika semina hiyo na washiriki wengine.

Mwenyekiti wa KIWAMATA Lauden Mwambona akizungumza na Jane Mihanji kutoka gazeti la Uhuru wa nne kutoka kulia ni Mkurugenzi wa www.fullshangweblog.com Bw. John Bukuku.

Mkurugenzi wa www.fullshangweblog.com Bw. John Bukuku akifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo.

Washiri wakifuatilia mada katika semina hiyo

Umakini ulikuwa ni muhimu ili kuelewa vizuri mada hizo.

Hapa ni baada ya Kushoo Love kwa picha ya pamoja

Hapa katika picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...