Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, August 31, 2012

MZEE YUSSUF AFUNGUA KAMPUNI YA USAMBAZAJI WA KAZI ZAKE

Meneja Mauzo wa Kampuni ya  Usambazaji ya MY CollectionMUSSA MSUBA akiwa katika duka la mauzo ya kazi za Jahazi
MSANII WA MZIKI WA TAARABU,MZEE YUSUFU KUSHOTO AKIANGALIA MOJA YA KAZI YAKE ILIYOKUWA FEKI ZILIZOKAMATWA NA WASANII WENYEWE KWA KUSHIRIKIANA NA KAMPUNI YA STEPS ENTANTAINMENT YA JIJINI DAR ES SALAAM
DVD ZA JAHAZI
MUSSA MSUBA

Na Mwandishi Wetu

MSANII wa mziki wa Taarabu nchini Mzee Yussuf ameamua kufungua kampuni yake ya usambazaji ijulikanayo kama MY Collection kwa ajili ya kusambaza kazi zake

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Meneja Mauzo wa Kampuni hiyo Mussa Msuba amesema wameamua kufungua duka kwa ajili ya kuuza CD NA DVD za bendi ya Jahazi inayongozwa na Mzee Yussuf duka hilo lililopo makutano ya barabara ya likoma na Muhonda

linalojihusisha na huzwaji wa DVD za taarabu kwa jumla na rejareja kwa ajili ya kuwaweka karibu wapenzi wake ili waweze kupata burudani kupitia nyimbo zao kwa kuwaburudisha wakiwa majumbani

Msuba amesema kuwa Mzee yusufu yupo mbioni kutoa albamu yake ya mduara itakayokuwa hivi karibuni ambayo ni yake binafsi mbali na hilo bendi hiyo itatoa video yake ya Live za albamu zake zote za Two in One,Kazi ya Mungu, Nakula ka Naksh Naksh,tupendane,Daktari wa Mapenzi

Ambazo zitakuwa madukani kwa ajili ya kuwapa wapenzi wao burudani wakiwa majumbani mwao

Nae Mzee Yussuf aliongeza kwa kusema ameanzisha Kampuni yake binafsi baada ya kuona kwamba kazi zake nyingi zimekuwa zikichakachuliwa kutokana na kuwepo kwa wizi wa kazi za Sanaa

Kampuni yake imekuwa ikisambaza kazi zake kwa ajili ya kuogopa kuibiwa kutokana na wimbi wa kazi za wasanii nchini

Duka lililopo mtaa wa Muhonda na Likoma kwa ajili ya CD za Jahazi pekee  mbali na duka hilo mzee Yusufu anamiliki Duka lingine la Nguo lililopo Magomeni Mapipa kwa ajili ya kujiongezea kipato chake mbali na bendi yake

Bendi ya Jahazi mpaka sasa imekwisha toa albam nane ambazo zipo madukani zinauzwa kwa ajili ya watu wotekupata burudani wakiwa majumbani mwao

Kwa sasa bendi hiyo ipo mbioni kuachia albamu yake ya tisa ambayo aijapewa jina inatarajiwa kuzinduliwa mwezo October kwa ajili ya kutoa burudani kwa wapenzi wao na kuwataka mashabiki wao kuja kuangalia na kusikiliza nyimbo mpya popote pale wanapotoa burudani zao katika kumbi mbalimbali za jijini Dar es salaam


DUKA LA MZEE YUSSUF LILILOPO KATIKA MAKUTANO YA MTAA YA LIKOMA NA MUHONDA LINALOSAMBAZA KAZI ZA BENDI YA JAHAZI

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...