Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, March 24, 2014

AS Vita yaifyatua Kaizer Chiefs 3-0


http://www.michezoafrika.com/NewsImages/VIta-club-of-Congo.jpg
KLABU YA AS Vita ya DR Congo imeifumua Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa mabao 3-0 katika mechi za 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika, huku AC Leopards ya Kongo ikilazimishwa sare nyumbani na Al Hilal ya Sudan.
mabao yote ya Vita katika pambano hilo yalifungwa na Firmin Ndombe Mubele na kuiweka katika nafasi nzuri timu yake ya kufuzu robo fainali ya michuano hiyo iwapo itakomaa kwenye mechi ya marudiano wiki ijayo nchini Afrika Kusini.
Katika michuano ya Kombe la Shirikisho, Zesco ya Zambia ikiwa ugenini nchini Ghana imechezea kichapo cha mabao 2-0 toka kwa wenyeji wao Medeama, huku Ismailia ya Misri na Petro du Luanda ya Angola zikishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu.
Nayo timu ya Warri Woriors ya Nigeria imelazimishwa sare tasa na Bizertin ya Tunisia katika pambano jingine la mkondo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho.
Mechi nyingine za ratiba ya mkondo wa kwanza zinaendelea kuchezwa kwa sasa ukiwamo pambano la TP Mazembe dhidi ya wenyeji wao Sewe Sports ya Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...