Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, March 18, 2014

Ruvu Stars waachia tatu, wajipanga kurekodi video


Roggert Hegga enzi akiwa Twnaga Pepeta
BENDI mpya wa muziki wa dansi ya Ruvu Stars, imekamilisha kurekodi nyimbo zao tatu mpya na tayari wameanza kuzisambaza kwenye vituo vya redio kwa ajili ya kuchezwa hewani.
Mmoja wa viongozi na muimbaji wa bendi hiyo yenye maskani yake Mlandizi, Pwani Rogert Hegga 'Catapillar', alisema wamemaliza kurekodi nyimbo hizo katikati ya wiki iliyopita na tayari baadhi ya vituoi zimeanza kuzirushwa hewani wakijiandaa kurekodi video zake.
Hegga alizitaja nyimbo zilizorekodiwa ambazo ndizo zinazoitambulisha bendi hiyo kwa mashabiki wa muziki wakiwa wanataka kurejesha enzi za bendi za majeshi kutamba nchini ni pamoja na 'Network Love' utunzi wa  Mhina Panduka 'Baba Danny' a.k.a Toto Tundu, 'Jua Kali' wa Kuziwa Kalala na 'Spirit' ambao ni utunzi wake (Hegga).
"Tumeshakamilisha kurekodi nyimbo zetu za utambulisho na tumeshasambaza na baadhi ya vituo zimeanza kuzicheza," alisema Hegga.
Mtunzi na muimbaji huyo wa zamani wa bendi kadhaa maarufu nchini ikiwamo ya African Stars, Mchinga Sound, G8 Wana Timbatimba na Extra Bongo, alisema vibao hivyo ni mwanzo wa maandalizi ya kupakua albamu yao na kuwataka mashabiki wasubiri kupata uhondo zaidi.
"Mashabiki wajiandae tu kupata burudani, nyimbo hizi zitaleta mapinduzi makubwa katika muziki wa dansi kwani zimeenda shule na studio tuliyorekodia ni bab'kubwa," alisema.
Baadhi ya wanamuziki wanaounda bendi hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ni Khadija Mnoga 'Kimobitel', Hamis Amigolas, Hegga, Victor Mkambi, Mhina Panduka na wengine waliotoka bendi kadhaa za jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...