Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, March 15, 2014

RIDHIWANI AANZA HARAKATI ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE


Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014. 
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akinong'onezwa jambo na Mmoja wa kinamama wa Kijiji cha Matipwili (Jina lake halikuweza fahamika mara moja).
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wanakijiji wakazi wa Kijiji cha Mkange,Saadani Wilayani Bagamoyo waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza huku wengi wakiahidi kumpa kura zao pindi itakapofika siku ya Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...