Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, March 24, 2014

Jahazi la Ashanti Utd lazidi kuzama, yapigwa 2-0


* Mgambo JKT yakomaa Mkwakwani
Ashanti waliyonyukwa 2-0 na Ruvu Shooting

Mgambo waliokomaa Mkwakwani na kutoka sare ya Mtibwa Sugar
Ruvu Shooting walioinyoa Ashanti Utd
TIMU ya soka ya Ruvu Shooting imeutumia vyema uwanja wake wa nyumbani baada ya kuifumua Ashanti Utd kwa mabao 2-0 katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku Mgambo JKT ikibanwa nyumbani na Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Mkwakwani-Tanga.
Elias Maguli ambaye alikuwa hajafunga bao lolote tangu duru la pili lianze alifunga bao la kwanza katika dakika ya sita na kuongeza jingine katika dakika ya 63.
Hata hivyo Ruvu iliyokuwa kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi walijikuta wakicheza pungufu baada ya mchezaji wao Ali Kani kutolewa kwa kadi nyekundu.
Ushindi huo umeifanya Ruvu kufikisha jumla ya pointi 31 na kushika nafasi ya sita pointi moja dhidi ya Kagera Sugar wanaokamata nafasi ya tano.
Katika mechi ya Mkwakwani, Mgambo na Mtibwa zilitoka sare ya 1-1 katika pambano linalodaiwa lilikuwa kali.
Wenyeji walitanguliwa kufungwa bao na Vincent Barnabas kabla ya kuchomoa baadaye kupitia kwa Peter Malianzi na kufanya mchezo huo kuisha kwa sare ya 1-1 na timu zote kuambulia pointi moja kila moja.
Katika pambano hilo mshambuliaji nyota wa Mgambo, Fully Maganga aliwaweka roho juu mabeki wa Mtibwa kwa muda mrefu wa pambano hilo licha ya kwamba hakufanikiwa kufunga bao kwa kukosa bahati siku ya leo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...