Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, August 25, 2010

BIA YA KILIMANJARO YAINGIA MKATABA WA MIAKA MITATU YA UDHAMINI WA BONGO STAR SEACH


Mkurugenzi wa BenchMark Production,Madame Ritha Paulsen akiongea leo katika ukumbi wa hoteli ya Paradise uliopo ndani ya jengo la Benjamin Mkapa wakati wa utambulisho wa mdhamini mkuu mpya wa Bongo Star Search ambaye ni kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chak cha Kilimanjaro premium lager.kushoto ni Meneja wa bia ya Kilimanjaro,George Kavishe na kulia ni Afisa masoko na mafunzo wa TBL,Edith Bebwa.

Bongo star search ni moja ya kipindi kinacho rushwa na television hapa nchini Tanzania ambacho kime fanikiwa kwa kiwango kikubwa kabisa kuinua vipaji vya wanamuziki wa Tanzania.

Ikumbukwe kuwa mwaka jana kampuni ya kutengeneza bia hapa nchini TBL kwa kupitia kinywaji chake kinachojihusisha na maswala ya muziki Kilimanjaro premium lager. Ilishiriki kama mmoja wa wadhamini wa shindano hilo.

Uhusiano huu mkubwa wa kampuni hizi mbili umetokana na sababu kuu kwamba BSS inahusika kutafuta na kuinua vipaji vya wanamuziki hasa vijana wa umri wowote ambapo Kilimanjaro premium lager kufuatia kauli mbiu yake ya Kufikisha Muziki wa Tanzania Kilele cha mafanikio kwa upande mwingine ina husika na muziki wa vijana wa Kitanzania.

Kilimanjaro premium lager imekua ikunga mkono juhudi za kuendeleza Muziki hapa Tanzania kwa kiwango cha juu.. Ikiwa mdhamini mkubwa kwenye zoezi la kutoa Tunzo za Muziki Tanzania kila mwaka,Tunzo zinazojulikana kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Ndio maana Kilimanjaro premium lager imeona hakuna sababu ya wao kutoshirikiana na BSS 2010 katika kuinua vipaji vya wanamuziki wa Tanzania.

Kilimanjaro premium lager imeandikisha mkataba wa kuwa mdhamini wa Bongo star search kwa kipindi cha miaka mitatu ambayo ni BSS 2010, BSS 2011, BSS 2012.

Washiriki wa BSS watashirikishwa katika mambo mbali mbali yakiwemo mashindano yatakayo kua yanafanyika siku hadi siku katika jumba la BSS KILI HOUSE 2010.

BSS 2010 itakuwa ikirusha hewani kila jumapili saa tatu na robo usiku (3:15) kupitia television ya ITV ikishirikiana na Radio one na magazeti ya The Guardian ,Nipashe.
unatakia kufuatilia shindano hilo bila kukosa na pia ni muhimu kupiga kura yako ili kuweza kuwachagua watakao weza kushiriki mpaka mwisho .

shiriki nasi ili kuweza kukamilisha ndoto za wanamuziki wetu.

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe akitangaza udhamini miaka mitatu wa shindano la Bongo Star Search katika hafla iliyofanyika katika hoteli ya Paradise jijini Dar es Salaam leo mchana. Kulia ni Mkurugenzi wa Benchmark Production, Ritta Paulsen.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...