Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, November 14, 2011

BAADA YA KUWAPA KUCHAPO CHAD TAIFA STARS WAWASILI NYUMBANI


Kocha wa timu ya taifa Taifa Stars Jan Paulsen akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo, mara baada ya timu hiyo kuwasili ikitokea N'Djamena nchini Chad, ambako ilicheza na timu ya taifa ya nchi hiyo na kuifunga magoli 2 kwa 0. Timu hizo zitarudiana siku ya jumanne wiki hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Taifa Stars inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili kuingia katika hatua ya makundi kwa ajili ya kinyang'anyiro cha kushiriki kombe la dunia mwaka 2014 nchini nchini Brazil.
Kulia ni Mchezaji wa Taifa Stars Nizar Khalfan na kushoto ni Henry Joseph wakiongoza wenzao wakati walipowasili kwenye uwanja wa ndege wa mwalimu J.K.Nyerere leo jijini Dar es laam wakitokea nchini Chad.
Kocha wa timu ya taifa Taifa Stars Jan Paulsen akiingia kwenye basi la timu hiyo, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere DIA jijini Dar es salaam.
Golikipa watimu ya taifa Juma K. Juma akiwa katika pozi katika basi la Taifa Stars leo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweriers (SBL) Teddy Mapunda na Meneja wa kinywaji cha Serengeti Lager Allan Chonjo kushoto, wakiwapongeza wachezaji wa Taifa Stars, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo alasiri.
Mwandishi wa habari wa BBC nchini David Eric Nampesya akimhoji katibu mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Angetile Osiah wakati wa mapokezi ya Taifa Stars iliyowasili nchini leo ikitokea nchini Chad.
Mwandishi wa habari wa BBC nchini David Eric Nampesya akipozi kwa picha na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweriers (SBL) Teddy Mapunda.
Mzungu huyu ambaye hakufahamika jina lake mara moja, akipata taswira baada ya kuvutiwa na vijana hawa wanaofanya kazi ya promosheni ya bia ya Serengeti Lager.
Wachezaji hawa wa kesho nao wameshiriki kuwapokea kaka zao Taifa Stars wakati walipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo.
Mashabiki mbalimbali wamejitokeza kuja kuwapokea wachezaji wa timu yao Taifa Stars ilipowasili leo ikitokea nchini Chad.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...