Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, November 12, 2011

TAARIFA YA KUPIMA UZITO NA AFYA WACHEZAJI NA WAAMUZI

TAARIFA YA KUPIMA UZITO NA AFYA WACHEZAJI NA WAAMUZI

BOXING FEDERATION OF TANZANIA (BFT)
SHIRIKISHO LA NGUMI TANZANIA
SLP 15558
DA ES SALAAM
12/11/2011
VYOMBO VYA HABARI.

YAH; TAARIFA YA KUPIMA UZITO NA AFYA WACHEZAJI NA WAAMUZI
WATAKAOSHIRIKI MASHINDANO YA KOVA CUP 14/11/2011
PR STADIUM HOTEL..
SHIRIKISHO LA NGUMI TANZANIA(BFT)LIMEPEPANGA KUWA UPIMAJI WA AFYA NA UZITO KWA WACHEZAJI NA WAAMUZI WATAKAO SHIRIKI KATIKA MASHINDANO YA KOVA BOXING CUP UTAFANYIKA TAREHE 14/11/2011 SAA 1.00 HADI SAA 4.00 ASUBUHI ,PR STADIUM HOTEL KATIKA UKUMBI WA HOTEL HIYO WA IJUMBI GRILL.

UPIMAJI WA AFYA NA UZITO UTASIMAMIWA NA WAAMUZI WALIOTEULIWA NA CHAMA CHA WAAMUZI WA NGUMI TANZANIA WAKISIMAMIWA NA KATIBU WAO JUMA SELEIMAN.

JUMLA YA WAAMUZI 8 NA DAKITARI 1 WAMETEULIWA KUJA KUCHEZESHA MASHINDANO HAYO BAADHI YAO NI JUMA SULEIMANI,SALEHE MWINYIKHERI,MANENO OMARI,RIDHAA KIMWELI,MARCO MWANKENJA,MAFURU MAFURU,MOHAMED BAMTULAH ,MOSHI MAKALI NA DAKITARI JOSEPH MAGESA,

ZAIDI YA TIMU 15 ZIMETHIBISHA KUJA KUSHIRIKI MASHINDANO HAYO BAADHI YA TIMU HIZO NI ASHANTI YA ILALA,NGOME, JKT,MAGEREZA,URAFIKI,MABIBO ,SIFA,MBAGALA,MIEMBENI,NDAME,MBEZI,LUAHA ,TEMEKE,KEKO,POPUILAR NA TIMU ILIYOOMBA KUSHIRIKI KUTOKA DODOMA

Katika Michezo hiyo ya siku mbili kutakua na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo Rajabu Mhamila 'Super D Boxing Coach' kabla ya kwenda kuhudhulia kozi ya kimataifa ya mchezo huo ambayo itaongozwa na mkufuzi ambaye ameteuliwa na Chama cha Ngumi cha Dunia (AIBA) Ndg Azzedin Aggoune kutoka Algeria
DVD HIZO kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi. Super D alisema katika DVD hizo kutakuwa na mapambano mengi ambayo yanaweza kutumika kama mafunzo muhimu kwa mabondia ,makocha marefa pamoja na mashabiki wa mchezo kujua sheria mbalimbali. '' Kuna mapambano kama ya akina Amir Khan, Manny Paquaio, Floyd Maywhether, David Haye, Mohamedi Ali pamoja na mtanzania Roja mtagwa anaefanya shughuli zake Marekani, DVD hizo ni nzuri na hata walio tayari tayali katika mchezo huo wanatakiwa kujua sheria na mafunzo ya ngumi mana zinafundisha mambo mengi '' alisema Super D DVD hizo za mafunzo zinapatikana makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au katika kambi ya ngumi ILala na klabu ya AShanti nayo ya Ilala.
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
Email.superdboxingcoach@gmail.com
www.burudan.blogspot.com
Mob;+255787 406930
+255774406938
Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

--

MAKORE MASHAGA
KATIBU MKUU BFT



No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...