Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, April 18, 2013

MAZIKO YA BI KIDUDE


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,alipohudhuria nyumbani kwa Marehemu Bi Fatma Baraka (KIDUDE) kuhani kwa Familia ya marehemu leo asubuhi Rahaleo Mjini Unguja. (Picha na Ramadhan Othman, Ikulu)
 Akina Mama mbali mbali waliofurika katika maziko ya Msanii Maarufu Marehemu Bi Fatma Baraka (KIDUDE)huko nyumbani kwake Rahaleo mjini Unguja leo.
Maelfu ya wanannchi na waislamu waliofurika katika msikiti wa Mwembr shauri katika maziko ya Marehemu bikidude leo,na kuzikwa kijini kwao Kitumba Wilaya ya Kati Unguja.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,(wa nne  kushoto) akijumuika na viongozi na waislamu katika kumswalia Marehemu Msanii maarufu Fatma Binti Baraka (kidude) katika msikiti wa Mwembeshauri Mjini Unguja leo.

 Vijana waliobeba Jeneza la mwili wa Marehemu Msanii maarufu Fatma Binti Baraka (kidude) wakati wa maziko yake yaliyofanyika leo huko kijijini kwao Kitumba,Wilaya ya Katri Unguja,ambapo maziko yake yamehudhuriwa na wasanii mbali mbali ndani na nje ya nchi. 
 Baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika maziko ya marehemu Bi Fatma Baraka (Kidude)  kijijini kwao Kitumba,Wilaya ya Katri Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,(kutoka kulia) Rais wa  jamhuri ya Muungano Dk. Jakaya Mrisho Kikwete,Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif,na Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi,wakiitikia dua baada ya maziko ya Msanii maarufu Fatma Binti Baraka (kidude) aliyefariki jana na kuzikwa leo Kijijini kwao Kitumba,Wilaya ya Kati Unguja.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...