Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, July 26, 2010

TTCL KUJIULIZA SHIMUTA SEPT ARUSHA


TTCL WAKIWA WAMEBEBA BANGO
TTCL WAKIWA UWANJANA NA CBE
wafanyakazi wa TTCL wakifulaia bonanza

TIMU ya netbol ya Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) mwishoni mwa wiki ilishindwa kufua dafu baada ya kupata kichapo cha mabao 12.6 kutoka kwa timu ya Chuo cha Biashara (CBE) katika Bonanza lililoyakutanisha mashirika na makampuni mbalimbali lililoandaliwa na (SHIMUTA)

Akizungumza katika viwanja vya Chuo Kikuu cha DAr es salaam baada ya kupata kipigo Ofisa Habari wa kampuni ya TTCL Amanda Luhanga, amesema kampuni hiyo imepata changamoto baada ya kichapo hicho ambapo hitakuwa kama chachu ya kuanzisha timu ya kudumu katika kampuni hiyo

;Unajua tangu kampuni ibinafsishwe hatukuwa na timu pamoja na kufungwa tunaona bado tuna huwezo wa kushindana katika michuano mingine itakayokuja mbele yetu tuna huwakika tukifanya mazoezi ya kutosha na kujipanga kama timu tutaludisha historia yetu ya kimichezo ; alisema Luhanga

Amesema kuwa mikakati ambayo TTCL ITAIWEKA NI PAMOJA NA KUWANOWA WAFANYAKAZI KATIKA MICHEZO MBALIMBALI PINDI AMBAPO WATAKAPOTENGA MUDA WA MAZOEZI ILI KUWEZA KUFANYA VIZURI;

'Tunataka tuwe na vikosi kazi ambavyo vitashiriki rasmi katika mashindano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi (SHIMUTA) alisema mashirika yaliyoshiliki bonanza hilo ni pamoja na TTCL,CBE,PSF,TBC,COCA COLA,ARDHI,BANDARI NA BIMA YA AFYA

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...