Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, July 7, 2010

VIOLET MZINDAKAYA SISTA V KUGOMBANIA UBUNGE VITI MAALUMU RUKWA



SISTA V
AKITOA SHUKLANI KWA WASANII KWA KUMPA SAPOTI
Mwanamziki wa kizazi kipya Abwene Yesaya akimkabidhi shilingi laki moja kwa Katibu msaidizi wa Idara ya Itikadi na Uwenezi pia ni Mjumbe wa NEC Chama cha Mapinduzi CCM, Violet Mzindakaya kwa ajili ya kwenda kuchukulia fomu ya kugombea ubunge wa viti maalumu mkoa wa Rukwa pesa hizo zimetolewa na wasaniaa Hamisi Mwijuma 'mwana FA na Abwene Yesaya AY kwa ajili ya kumpa sapoti kijana mwenzao ili aende kuwawakilisha vema bungeniMSANII wa Muziki wa kizazi kipya nchini Ambwene Yesaya 'AY' na Hamisi Mwinjuma 'Mwana FA', kwa pamoja wamemchangia sh. 100,000 mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Chama cha Mapinduzi CCM (NEC) Violet Mzindakaya 'Sister V' kwa ajili ya kuchukua fomu ya ugombea wa nafasi ya viti maalum Mkoa wa Rukwa.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mchango huo AY alisema, wao wamehamasika kumchangia kutokana na kwamba ni kijana mwenzao na kwamba anajua matatizo ya vijana hivyo atawakilisha vyema matatizo ya vijana Bungeni.

"Tumeamua kwa pamoja kutoa mchango huu kwa mwenzetu ili kuweza kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo pia tunawaomba na watu wengine ambao wanaona yupo mtu atakayeweza kuwawakilisha vyema kutoa mchango wao kama tulivyofanya sisi,"alisema AY.

Kwa upande wake sister V amewashukuru na kuwapongeza wasanii hao kwa kuonesha na kuahidi atawawakilisha vijana wote vema pindi atakapopata nafasi ya kuchaguliwa ya kuingia Bungeni.

Sister V ambaye pia alikuwa mtangazaji wa avituo mbalimbali vya redio nchini ikiwemo KItuo cha redio cha 100.5 Times FM, redio Uhuru na Clouds FM amewaomba watanzania kumuunga mkono ili aweze kufanikiwa na kutimiza malengo ya vijana wote.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...