Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, June 24, 2013

Ommy Lax, PNC kupotezea videoni


Ommy Lax
MSANII anayekuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya Iman Omar 'Ommy Lax' anajiandaa kurekodi video ya wimbo wake mpya uitwao 'Wapotezee' alioimba na mkali wa Watanashati, PNC.
Akizungumza na MICHARAZO, Ommy Lax alisema kuwa maandalizi ya kuanza kurekodi video hiyo imekamilika na kwamba zoezi hilo litafanyika wiki hii katika maeneo mbalimbali ya jijini Dar es Salaam.
Ommy Lax alisema kuwa 'audio' wa kibao hicho tayari imeanza kurushwa hewani na ameona ni vyema kukata kiu ya mashabiki wake kwa kuwatengenezea video ili waone kwa ukamilifu ujumbe wa wimbo huo.
"Baada ya kuachia 'audio' kwa sasa nafanya maandalizi ya kurekodi video ya wimbo wangu uitwao 'Wapotezee' ambao nimeimba kwa kumshirikisha PNC, nimepanga kurekodi wiki ijayo ili niisambaze mapema," alisema Ommy Lax.
Hicho ni kibao kingine toka kwa msanii huyo ambaye anatamba na wimbo wa Kioo Changu alioimba na Matonya 'Tonya Business'.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...