Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, December 22, 2012

TDL YAZINDUA KINYWAJI KIPYA CHA ZANZI CREAM LIQUEUR JIJINI DAR LEO.




 

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL),David Mgwassa akisungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa kinywaji kipya kinachoitwa ZANZI (kinachoonekana pichani) iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena,jijini Dar es Salaam leo.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL),Joseph Chibehe akitoa ufafanuzi wa Kinywaji hicho kipya aina ya ZANZI ambacho kinapatikana katika ujazo wa 750ml na katika Pakiti zenye ujazo wa 100ml ambacho kitakuwa kikipatikana nchi nzima.Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya TDL,David Mgwassa na kulia ni Meneja Usafirishaji wa TDL,Bavon Ndumbati.
"...hiki ndicho kinywaji kipya tulichokizindua leo..."
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL),David Mgwassa (katikati),Meneja Masoko wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL),Joseph Chibehe na Meneja Usafirishaji wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL),Bavon Ndumbati wote kwa pamoja wakigonganisha glass kuashiria uzinduzi rasmi wa kinywaji hicho uliofanyika leo kwenye hoteli ya Serena,jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...