Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, October 31, 2013

AIRTEL MONEY HAKATWI MTU INAWAPIGA TAFU WAFANYA BIADHARA YA SAMAKI MWALONI MUSOMA NA MWANZA.


 kushoto ni Meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando na kulia ni Ofisa
Masoko wa kanda ya ziwa Bw Ally Mashauri wakimkabidhi vitendea kazi
vya uwakala Bw, Innocent Godwin (kati) anaefanya uwakala ndani ya soko
la samaki la kimataifa Mwaloni Kirumba Mwanza leo wakati ambapo airtel
walitembelea sokoni hapo kujionea jinsi wauzaji na wanunuzi wa samaki
wanavyoitumia huduma yao ya  kutuma na kutoa pesa bila makato
wanapokuwa kwenye biashara zao-hakatwi mtu hapa
 Wakwanza mbele kushoto ni Meneja uhusiano wa Airtel jacksonm Mmbando
na ofisa masoko wa Airtel Mwanza Bw Ally Mashauri wakimsikiliza bw,
Rashid Moshi mmoja wa wauzaji na mvuvi wa samaki katika soko la
kimataifa la Samaki Mwaloni Kirumba Mwanza leo wakati ambapo Airtel
walitembelea sokoni hapo na kuzungumza na wateja wao jinsi huduma ya
Airtel Hakatwi mtu inavyowafaidisha kufanya biashara zao za kuuza na
kununua samaki kupitia airtel money bila makato- Hakatwi mtu hapa.


Biashara ya samaki kwenye Mwalo wa Musoma mkoani Mara na Kirumba
mkoani Mwanza imepata msukumo wa kipekee baada ya kuanzishwa kwa
kampeni ya hakatwi mtu, ambayo inawawezesha watumiaji wa mtandao wa
airtel kutuma na kupokea pesa bila makato.

Ikiwa inaingia katika mwezi wa tatu sasa kampeni ya hakatwi mtu
inayowawezesha wateja wa airtel money kufanya miamala yao bila makato,
wafanyabiashara na wachuuzi kwenye soko la samaki la Mara Mmusoma
wanatumia kampeni hiyo kama njia ya kupunguza kutembea na pesa muda
wote kwa ajili ya kununua ama kuuza samaki na dagaa

mwenyekiti wa soko la samaki na dagaa mwaloni Musoma Mara bw, Gideon
Dogori anasema airtel money hakatwi mtu ni sawa na kufanya biashara ya
malipo kamili yaani cash kutokana na falsafa yake ya hakatwi mtu.

Anasema wafanyabiashara sokoni hapo hufanya malipo kwa kutumia airtel
money na hawana tena ulazima wa kutembea na maburungutu ya fedha kwa
ajili ya kununulia dagaa ama samaki.

"Tangia hawa jamaa wa airtel waanzishe hii huduma yao ya hakatwi mtu
wafanyabiashara hapa wamekua hawatembei na lundo la hela kama
ilivyokua mwanzoni bali sasa wanauza na kununua bidhaa kwa kutumia
simu zao za mkononi",alisema Bw. Dogori.

"Kuna wengine wanaishi nje ya Musoma kwahiyo wanatuma tu pesa na
wanatumiwa bidhaa zao huko walipo bila kufika hapa sokoni kwasababu
huduma ya airtel money haina makato yoyote" aliendelea kueleza
mwenyekiti wa mwalo wa samaki na dagaa musoma bw. Dogoli.

Bw Dogori anasema faida kubwa inaonekana kwenye huduma hii hasa kuokoa
muda kwa wafanyabiashara, ambapo hawahitajiki kusafiri mwendo mrefu
kwenda sokoni hapo kufanya manunuzi kama ilivyokuwa zamani bali
wanatuma tu hela na kusubiria bidhaa zao huko walipo.

"Huduma hii ingekuwa ya kudumu ingesaidia sana wafanyabiashara kwani
ka muda huu mfupi imeweza kusaidia kuongeza hata miataji kwa
wafanaybiashara hapa mwaloni", alisisitiz Dogori.

Bi Mkami Magesa ni mfanyabiashara kwa zaidi ya miaka kumi sokoni hapo,
anasema wakati huu biashara imerahisishwa sana kwani kupitia huduma ya
hakatwi mtu amekuwa akifanyabiashara kubwa na anapata pesa yake bila
makato.

"Hii huduma ya airtel money ya hakatwi mtu ni mkombozi kwakweli kwani
mteja anaweza akawa shinyanga ama singida anatuma humu pesa na mimi
nampakilia mzigo wake anaupata bila ya yeye kufika hapa mwalini",
alisema bi Mkami.

Kwa upande wake John Anton  mchuuzi wa dagaa na samaki katika  soko la
samaki Mwaloni Mwanza Anasema anachofanya ni kutoa oda ya bidhaa
anazohitaji na kisha kutuma pesa bila makato kwenda kwa muuzaji na
kuokoa muda wa kusafiri kutoka sirali anapoishi na kufanyia biashara
zake.

"Kwasasa maisha na biashara imekuwa rahisi sana nawaomba airtel
kuifanay huduma hii kuwa endelevu maana inasaidia sana katika shughuli
za kibiashara", alisema Bw. Bundala.

Bw Dogori ambaye ni mwenyekiti wa mwaloni mjini Musoma alimalizia kwa
kusema elimu zaidi ya matumizi ya huduma za airtel money inahitajika
kwani zimeanza kuonesha dalili za kuwa mkombozi kwa wafanyabiashara wa
soko lake.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...