Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, October 31, 2013

PHD AOMBA RADHI MASHABIKI




Na Elizabeth John
MSANII wa filamu na bongo fleva nchini, Hemed Suleiman ‘PHD’ amewaomba radhi mashabiki wa muziki wake kwa kutoonekana msanii, Heri Samir ‘Mr Blue’ katika video ya wimbo wake wa ‘Rest Of My Life’.
Katika video ya wimbo huo, sauti ya Mr Blue unasika lakini yeye haonekani kitu ambacho kimewashangaza mashabiki wa msanii huyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Hemed alisema hiyo imetokana na msanii huyo kutokuwepo nchini wakati akifanya ‘shooting’ ya wimbo huo.
“Naomba sana radhi kwa mashabiki wangu kwa kutoonekana Mr Blue katika video ya wimbo huo, wakati nafanya video ya wimbo huo, hakuwepo nchini baada ya kuona audio imekaa kwa muda bila video nikalazimika kuifanya pekeyangu,” alisema.

Msanii huyo alishawahi kutamba na kazi zake kama, ‘Mama Kimbo’, ‘Usiniache’, ‘Ninachotaka’ na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki huo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...